ALICHOSEMA RAIS WA ZANZIBAR KUHUSU VURUGU ZILIZOTOKEA.
habari za kitaifa 8:41 AM
Akizungumza na waandishi wa habari, wahariri na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk. SHEIN amesema kuwepo kwa mikutano yenye sura ya dini lakini inahusu masuala ya siasa hasa Muungano ni uvunjifu wa amani na ndiyo sababu iliyosababisha vurugu visiwani humo na kutaka jambo hilo lisijirudie kwani limeonyesha ubaguzi na kujenga hofu kwa wananchi.
Amesema amekuwa na utaratibu wa kukutana na viongozi wa dini mbalimbali na kuzungumza kuhusu masuala ya ulinzi wa amani na kubainisha kuwa ataendelea na utaratibu huo ili kuhakikisha Zanzibar inaendelea kuwa kisiwa cha amani.
“tumeshuhudia maandamano ya mikutano yenye sura ya dini lakini yenye ujumbe wa siasa, imefikia mpaka wameamua kuchoma moto majengo, wakachoma Makanisa ya ndugu zetu wakristo bila sababu yeyote ile, wamevunja maduka ya baadhi ya wenzetu raia wema, nimeshangazwa sana.. kuna uhusiano gani wa kuzungumzia muungano na kuchoma moto makanisa, kuiba vitu vya watu, kutukana na kutisha watu? haya ni kinyume na katiba yetu na sheria zetu” alisema Dr Chein.
kwenye sentensi nyingine Dk. SHEIN amewataka wananchi kutumia busara na kufuata taratibu zilizowekwa katika kutoa maoni ya katiba ili kuwezesha kupatikana kwa katiba bora kwa kurekebisha kasoro zilizopo.