BBC DIRA YA DUNIA KURUKA LEO KWENYE TV KWA MARA YA KWANZA


Saleem Kikeke

Matangazo ya televisheni ya Dira ya Dunia ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC leo yanaanza kuruka rasmi kupitia Star TV ya Tanzania na Qtv ya Kenya.

Wiki iliyopita kulifanyika uzinduzi wa matangazo hayo jijini Dar es Salaam.

Matangazo hayo ya Dira ya Dunia kwa upande wa radio ni maarufu zaidi pengine kuliko matangazo yote ya radio za kimataifa zinazotangaza Kiswahili duniani.

Kuingia kwenye matangazo ya runinga kwa BBC Swahili kunafungua ukurasa mpya wa matangazo ya aina hiyo ya Kiswahili nchini.

BBC Dira ya Dunia siku za usoni itakuwa ikishindana na matangazo mengine ya Kiswahili ya Al-Jazeera ambayo yapo kwenye mchakato wa kuanzishwa.

Posted by Bigie on 8:26 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.