CHEGE ADAIWA KUZAA NA MKE WA MTU



Msanii wa hit ya ‘Mkono Mmoja’ Chege Chigunda aka Mtoto wa Mama Said ametupiwa shutuma kali kuwa amemzalisha mke wa mtu.

Akiongea na U Heard ya Clouds FM leo, mume huyo aliyejitaja kwa jina la Jose mkazi wa Kasulu mkoani Kigoma amesema mke wake aitwaye Salma amejifungua mtoto anayefanana kila kitu na Chege.



Akizungumza kwa jazba, Jose amesema yuko tayari kwenda kuchukua vipimo vya DNA na kama vikionekana negative atamlipa Chege shilingi milioni tano.

Amesema kesho anaanza safari yake ya kuja Dar es Salaam kumleta Salma na mwanae kwa Chege ambaye anasema ndiye baba yake mzazi huku akitishia kumfanyiaa kitu mbaya staa huyo.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Chege aliyekuwa akiongea kwa dharau amesema hajui lolote na wala hamfahamu Salma.

Posted by Bigie on 9:14 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.