"SIJAWAHI KUFA NA KUFULIWA BALI YALIKUWA NI MAJINI TU YAKINIKABA"....LINAH



Estelina Sanga ‘Linah’.

MSANII wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Estelina Sanga ‘Linah’, amekuja juu akijibu madai kwamba, aliwahi kufa na kufufuliwa na Mchungaji  wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima kwa kumfanyia maombi.


Akizungumza na mwandishi wetu, Linah alisema hajawahi kukumbwa na tukio hilo zaidi ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kuzimia mara kwa mara na kuponywa kwa njia ya maombi na Gwajima.


“Kwenye maisha yangu sijawahi kufa na kufufuka, kama umesikia hivyo basi hayo yalikuwa ni maneno tu, hapo mwanzo nilikuwa na kitu kama masheteni yalikuwa yakinikaba na kunifanya nipoteze fahamu mpaka nilipoombewa na Gwajima,” alisema Linah.

Posted by Bigie on 12:54 AM. Filed under , , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.