"BORA NIUGUE MARALIA KULIKO UGONJWA WA MAPENZI MAANA HUNICHUKUA MUDA KUPONA".....JACK WA MAISHA PLUS



Mwanadada  aliyepata jina kupitia Shindano la Maisha Plus Season II, Jacqueline Dustan ‘Jack wa Maisha Plus’ ambaye kwa sasa anafurukuta kwenye filamu za Kibongo amefunguka kuwa ni mgonjwa kwenye mapenzi na kama ikitokea akasalitiwa anaweza hata kulazwa hospitali akiwa hajitambui.

Jack aliiambia mpekuzi  kuwa mara nyingi akimpenda mwanaume humpenda kisawasawa na pale anapotokea kusalitiwa anakuwa mgonjwa na hata chakula kinakuwa ni kigumu kupita katika koo kutokana na kuzimika katika dimbwi la mapenzi kupita maelezo.

  “Kwa kweli bora niugue malaria coz najua nitakunywa dawa then nitapona lakini sitaki kabisa kuugua ugonjwa wa mapenzi unanifanya nakonda na huwa inanichukua muda mrefu kupona.”..
JACK

Posted by Bigie on 7:58 PM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.