SALHA ISRAEL AVAMIWA USIKU.....GARI LAKE LANUSURIKA KUBEBWA


WATU wanaosadikiwa kuwa ni majambazi juzikati walivamia nyumbani kwa Miss Tanzania 2011, Salha Israel maeneo ya Sinza-Mori jijini Dar na kufanya jaribio la wizi.
Akizungumza na mwandishi wetu, Salha alisema tukio hilo lilijiri hivi karibuni mishale ya saa 8:00 usiku ambapo watu hao wasiofahamika waliruka ukuta na kutaka kufanya uhalifu lakini walishitukiwa kabla ya kutekeleza mpango huo.

“Sijui niseme ni wezi au majambazi ila ilikuwa saa 8 usiku, watu hao waliruka ukuta wakaingia ndani. Hutujui kama walitaka kuondoka na gari au kuiba vitu vilivyokuwemo ndani yake lakini walivunja kioo cha mbele.

“Kwa bahati tulisikia vurugu zao na kabla ya kuiba chochote, tuliwakurupusha na ndipo walipokimbia,” alisema Salha.

Posted by Bigie on 1:03 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.