SHILOLE ANUSURIKA KUKAMATWA NA POLISI BAADA YA KUHISIWA KUWA ANA MISOKOTO YA BANGI


MSANII wa anayefanya vizuri kwenye muziki na filamu Shilole, amenusurika kumakatwa na polisi baada ya kuhisiwa kuwa na misokoto ya bangi ndani ya gari lake na kusababisha kuhojiwa kwa dakika kadhaa maeneo ya Kinondoni.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana ambapo msanii huyo inadaiwa alikuwa akitokea kwenye ishu zake ndipo maafande hao wanaliokuwa wakitokea kwenye malindo yao walipomdaka na kumpeleka pembeni kwa lengo la kufanya upekuzi kwenye gari yake.


Inadaiwa kuwa polisi hao hawakukuta kitu chochote zaidi ya sigara za mpenzi wake, ambaye walikuwa wote usiku huo na hata hivyo hawakuwa na dalili zozote za kuwa wamelewa.


Shilole
alipozungumza na mwandishi wetu alidai kuwa tukio hilo lilimshangaza sana kwani hakuwa na bangi ndani ya gari lake na hajawahi kutumia kitu hiyo lakini polisi hao walimuhoji kana kwamba anatumia bangi.

Alidai kuwa kuna baadhi ya watu walitaka kumfanyia mchezo mchafu lakini walishindwa kwani alikuwa makini katika kila jambo ambalo alikuwa akilifanya usiku huo, na alipoulizwa kuwa usiku huo alikuwa anatoka wapi alidai kuwa katika harakati zake za hapa na pale.

Posted by Bigie on 11:27 PM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.