"NAFURAHI SANA KUWA NA MAKALIO YENYE AFYA".....SNURA MUSHI


MSANII anayefanya vizuri kwenye filamu na muziki Snura Mushi ‘Snura’, amekili wazi kuwa makalio yake yanaongezeka siku baada ya siku na hii inatokana na mavazi anayovaa, huku nguo nyingine zikimpa wakati mgumu hata anapotembea kutokana na kumbana sana.

Akiongea na mwandishi wetu ,msanii huyo alidai kuwa amekuwa akijishangaa kutokana na makalio yake kubandilka siku baada ya siku na kuongezeka kwa kiasi kikubwa, huku baadhi ya nguo alizokuwa anavaa baadhi zinambana na hawezi kuzitumia tena.

Alisema kuwa inawezekana kukua kwa  makalio yake kunatokana na kulizika kwani sasa hana mawazo kama aliyokuwa nayo miaka kadhaa nyuma......


Aliongeza kuwa hajawahi kutumia dawa za aina yoyote za kukuza makalio na kuhusu makalio yake kuongeza anaamini ni umbo lake hivyo anahisi baadhi ya watu wenye mawazo mafupi wataanza kuhisi anatumia dawa hizo hatari na hataki watu wamfikilie vibaya, wala kuhisi anatumia.

“Utashangaa kuona picha nyingi nazopiga sasa zinaonesha makalio yangu yamekuwa sana nashindwa kuelewa ni kwa nini ila naamini maisha yangu ya sasa hayana mawazo kama ya miaka kadhaa iliyopita .....


Nafurahi  sana  kuwa  na makalio  yenye  afya aliongeza.

Posted by Bigie on 11:29 AM. Filed under , , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.