MTANGAZAJI WA REDIO WA TANZANIA AKAMTWA NA MADAWA YA KULEVYA NCHINI KENYA




Hivi karibuni mamlaka nchini Kenya zilikamata madawa ya kulevya aina ya heroin yenye uzito wa kilo 5.44.

Msemaji wa mamlaka ya mapato nchini Kenya (KRA) Kennedy Onyonyi amesema madawa hayo yalikamatwa yakiwa na mtanzania Saraphia Peter Shirima, Jan. 23 alipokuwa akijaribu kuvusha madawa hayo kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.


Mamlaka hiyo imesema Saraphia sio mwanafunzi bali ni mtangazaji wa radio nchini Tanzania.Onyonyi alisema mtangazaji huyo ana kibali cha kuishi nchiini Sweden kwa miaka miwili kitakachoisha ” Nov. 28, 2014.

Madawa hayo yana gharama ya dola za kimarekani 150,000 ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa akiyasafirisha kuyapeleka Budapest, Hungary.

Posted by Bigie on 8:50 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.