MR. BLUE ATUPIWA VITU VYAKE NJE NA NHC BAADA YA KUFANYA "UFISADI" WA CHUMBA


Familia ya staa wa Bongo Fleva, Herry Samir ‘Mr. Blue’, imeingia kwenye kashikashi baada ya kuvunjiwa nyumba na kutupiwa vitu nje, Risasi Jumamosi linashuka nayo.

Tukio hilo lililoshuhudiwa na ‘mwandishi’ wetu lilijiri Januari 30, mwaka huu, Posta, jijini Dar katika Ghorofa ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambayo Mr. Blue alikuwa amepanga na ndugu zake akiwemo mjomba wake (jina halikupatikana).


Kwa mujibu wa chanzo makini, Mr. Blue na mjomba wake walipangisha chumba kimoja kwenye ghorofa hiyo kwa miaka mingi iliyopita kisha wakaamua kuiba chumba kingine ambacho kilikuwa hakina mpangaji.

“Walitoboa mlango kwenye chumba ambacho kilikuwa hakitumiki, wakaanza kukitumia bila kukilipia hivyo jamaa wa NHC walipotimba wakatoa vyombo vyote nje,” kilisema chanzo.


Ilifahamika kuwa siku ya tukio wamiliki (NHC) walivamia na kuvunja mlango kwa kuwa Mr. Blue hakuwepo na aliporudi alikuta zoezi la kutoa vyombo likiendelea.


Alipoulizwa na Mwandishi wetu aliyefika eneo la tukio, kuhusiana na sakata hilo, Mr. Blue alikiri kutolewa vyombo nje na kudai hakuna tatizo kwani alivipelekwa kwa mjomba wake.

Posted by Bigie on 2:26 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.