KING MAJUTO AFICHUA SIRI ZA KUANGUKA KWA FILAMU ZA VICHEKESHO


MCHEKESHAJI nguli hapa nchini, Amri Athuman ‘King Majuto’ ameweka wazi kuwa, wasambazaji wa kazi za sanaa wamechangia kwa kiasi kikubwa kuyumba kwa soko la filamu za vichekesho.

King Majuto aliyasema hayo jijini Dar es Salaam, katika mazungumzo maalum na Saluti5 juu ya maoni aliyonayo kuhusiana na maendeleo ya filamu za Komedi hapa nchini.

“Unajua, unaweza kuandaa komedi yako kwa hata zaidi ya milioni 7, lakini unapompelekea msambazaji anataka kuinunua kwa milioni 2,” alisema King Majuto.

King Majuto alisema kuwa, kutokana na hilo, waandaaji wengi hivi sasa wamekuwa wakitayarisha kazi zao katika kiwango kisichokidhi, ili kuepuka gharama na hasara na matokeo yake mashabiki wanafikia hatua ya kuzipuuza na kuzikimbia kazi zao.

Posted by Bigie on 10:07 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.