Maelfu ya Wamarekani warejea kazini baada ya bunge la Congress kukubali kuipitisha bajeti ya nchi hiyo


Maelfu ya Wamarekani wamerejea makazini kufuatia Bunge la Congress la nchi hiyo kupitisha bajeti ya nchi hiyo baada ya siku 16 za kukwama na kusababisha serikali kufunga baadhi ya shughuli zake.

Akizungumza katika Ikulu ya nchi hiyo baada ya kusaini muswada huo, Rais Obama amesema hatimaye tishio lililoudhoofisha uchumi wa Marekani sasa limeondoka.

Makamu wa Rais wa nchi hiyo Joe Biden, aliwatembelea wafanyakazi wa serikali walioonyesha kufurahia hatua hiyo ya wanasiasa katika maeneo mbalimbali ya ofisi za serikali.

Baadhi ya wafanyakazi hao, wamewalaani baadhi ya wanasiasa wa nchi hiyo kwa kuweka mbele maslahi binafsi badala ya kujali umma wa Wamarekani.


-Magic Fm 

Posted by Bigie on 4:32 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.