Dina Marious wa Clouds FM Aamua Kufunguka..Kumbe Amewekwa Benchi Kutangaza..
udaku 1:06 PM
Kupitia Ukurasa wake wa Instagram Mtangazaji Dina Marious Amefunga Mengi
kuhusa hali yake na nini kinaendelea kwenye Ajira yake baada ya muda
mrefu kuwa kimya:
Ameandika Haya:
'Katika haya maisha hamna kitu kibaya kama kumuonea na kumnyanyasa mtu
ambaye hana hatia.Kwa kutumia cheo,madaraka,nguvu na nafasi uliyonayo
ukiamini huyo mtu hana uwezo wa kukufanya lolote
Tunaishi katika dunia ambayo binadamu wamekosa utu na imani.Binadamu
wamekuwa wanyama na makatili kuliko wanyama wenyewe.Unaweza ukakutana na
simba na chui porini mkakaa mkatia story lakini sio binadamu.
Unafanyiwa unyama eti kisa wanataka revenge kwa mtu wako wa karibu.Ambae
revenge hiyo wala haimuathiri lolote zaidi ni kukutesa wewe
kisaikolojia siku hadi siku.
Mbaya zaidi sikustahili miaka yote nimejituma,nimejitoa,sijawahi kumvunjia heshima alokuwa juu yangu kwa ngazi zoote.
Ndugu zangu nimeishi kwa muda mrefu katika huzuni,msongo wa mawazo.Na
hapa niliponimedevelop na vidonda vya tumbo.Nimekuwa na kitu kifuani
kimenikaaa kila siku nahisi nisiposema nitakufa.Ningekuwa nimetendewa
haki isingeniuma wala kunisumbua ni kwa sababu nimeonewa sanaa tena
katika kipindi kibaya sana.
All this time nimekuwa mnyenyekevu na najichekesha nakujitabasamisha
machoni pa watesi wangu.Na wao wakiendelea kunikanyagia chini bila
huruma huku wakinichekea.
Leo nimeamka nina huzuni sana sana na ninahuzunika hasa ninapokutana na msg za kuniuliza niko wapi?mbona sisikiki??
Mimi bado ni muajiriwa na ninalipwa mshahara ila nimewekwa benchi tu.
Kuna kitu naomba nikiweke clear kumekuwa na maneno mengiiiiii
yanazunguka kuwa nina ugomvi na Zamaradi.Mimi sina ugomvi na Zamaradi
sijui ndio amechangia mimi kutolewa kwenye leo tena.Thats not true wala
nguvu hiyo hana.Sijajua why watu husema hivyo ila sina ugomvi nae.Hata
yeye anajua hatuna ugomvi wowote.Nilipotoka pale niliamua kubadili mfumo
wangu wa maisha hivyo hatuna ukaribu kama zamani.Ila haimaainishi tuna
ugomvi.
Na malizia kwa kusema sipo radio wala sipo tv kwa sasa.Maswali
mnaniuliza kila siku na nina wajibu kila mara na leo nimewajibu tena.
ila nitakuwa kwa radio na tv hapo baadae acha niuze mafuta ya
nazi.Maelezo ya mwanzo yamejitosheleza sanaa na sitaenda mbalii sanaa
labda nikiandike kitabu ndio yatatimia.
Nimeandika haya kwa ufupi mjue hata sisi pamoja na majina tuliyonayo
changamoto zipo na tunakabiliana nazo.Na ipo siku tutashinda maana
mtetezi wetu yu hai ' Dina Marious