LADY JAYDEE NA PROF JAY NDANI YA NGOMA MOJA YA "JOTO, HASIRA"
Posted by Bigie habari za kitaifa, lady jaydee, PROF.JAY, PROFESA JAY 3:17 AMProfesa Jay na Lady Jaydee wanapokutana siku zote huwa hapaharibiki kitu, ni hit tu. Baada ya miaka mingi kupita, nguli hao wamekutana tena na guess what, this time hakuna amani kabisa kati yao, ni Joto na Hasira tu.
Unakumbuka Profesa Jay ameshawahi kumshirikisha Jide kwenye nyimbo zake mbili zilizohit sana enzi zake, Bongo Dar es Salaam na Nimeamini? Lakini kumbukumbu zetu hazituambii kama tulishawahi kusikia wimbo ambao Lady Jaydee amemshirikisha Profesa Jay. Hivyo huenda huu ndio ukawa wa kwanza.
Kupitia Facebook jana Lady Jaydee aliandika:
Naomba ku share muonekano wa ndani wa CD ya wimbo wangu mpya “JOTO, HASIRA” feat Prof Jay ambao unatoka siku za karibuni.” Lady Jaydee aliwaomba mashabiki wake wamsaidie kuchagua kava la wimbo huo.
PROFESA JAY AMPA SHAVU VANESSA MDEE....ADAI KUWA KIPAJI CHAKE HAKINA MPINZANI
Posted by Bigie habari za kitaifa, PROFESA JAY, VANESSA MDEE 1:46 AMTangu aachie wimbo wake wa kwanza, Closer, Vanessa Mdee amekuwa akimwagiwa sifa kibao kutoka kwa watu mbalimbali kiasi ambacho kimewafanya baadhi ya watu wahisi kama anapendelewa. Lakini ni ukweli usiopingika kuwa mtangazaji huyu ameendelea kujipatia mashabiki kibao.
Shabiki wake mpya wa sasa ni heavy weight mc, Joseph Haule aka Profesa Jay.Profesa Jay ameshindwa kujizuia na leo kwenye mtandao wa Twitter amefunguka kwa Vanessa kwa kutweet, “ Vanessa Mdee una kipaji cha hali ya juu sana, nakuomba sana sana ukichukulie SERIOUS, maana nahisi kama bado unauchukulia MUZIKI kama HOBBY!”
“Coming from you. That means everything. Nashukuru, na nimekusikia. I’m serious about this thing. Asante,” alijibu Vanessa.
Naye Dj maarufu wa nchini Marekani ambaye hivi karibuni alikuja nchini, Dj Topsin alitweet kuusifia wimbo wake kwa kuandika, “Ayo @VanessaMdee, ‘Closer’ is crackin’. I’m feelin’ flavor overall & the usage of both languages. #WorldWideReach #SeeYouAtTheTOP.”
Hizi ni tweets zingine za radio na madj kutoka Rwanda na Kenya zinazousifia wimbo huo:
@Fifilyn: Tune in Kigali to Radio 10 for @VanessaMdee #CLOSER!!!! CHUUUUNNNEEEEE big up girl!!!
@xclusivedeejay: Kenyan djz look for closer by @VanessaMdee certified jam across borderz!!!I’ll be droppin it tonight at bacchus lounge…heavy tune.
PROFESA JAY AZUSHIWA KIFO....
Posted by Bigie habari za kitaifa, PROFESA JAY 9:52 AMKuna habari za uzushi zimesambaa leo kuwa rapper Joseph Haule aka Profesa Jay amefariki dunia ambazo kwa mujibu wake mwenyewe Profesa zimemshtua mama yake kwa kiasi kikubwa.
Taarifa hizo za uzushi zimedai kuwa Profesa Jay alianguka na kuzimia na wengine kudai amefariki.
Kupitia mtandao wa Twitter, Profesa Jay amezikanusha taarifa hizo kwa kuandika, “Jamani eeeh mimi ni mzima wa afya njema hao wanaozusha kuwa nimekufa wataanza wenyewe. Mi niko fresh mpaka natamani kujiteka.”
“Watu hawana kazi za kufanya kila siku kuwaombea wenzao mabaya tu maisha sijui yamewashinda wamekalia uzushi tu. Leo zamu yangu nimepigiwa simu mpaka nimeshangaa kumbe watu wanataka kuhakikisha mzee washindwe na walegee,” aliongeza.
“Imemshtua sana mama yangu maana alinisikia nilipokuwa nikioongea na moja ya simu zilizokuwa zinanipa ripoti hii.”
PROFESA JAY AKANUSHA KUMTAPELI PROMOTA WA MOMBASA
Posted by Bigie BONGO FLEVA, habari za kitaifa, PROFESA JAY 2:39 AMHivi karibuni gazeti la The Star a nchini Kenya liliandika kuwa rapper Joseph Haule aliingia kwenye mgogoro mkubwa na promoter wa mjini Mombasa Kenya aliyemchukua kufanya show na kumshutumu kuwa amemtapeli.
Prof alikuwa amechukuliwa kufanya show mbili siku ya Christmas kwenye kumbi za Jamboree Resort na Quetu Beach Resort.
Hata hivyo kwa mujibu wa website ya mtangazaji wa East Africa Radio, Sam Misago, Profesa amethibitisha kuwa taarifa hizo si za kweli.
Website hiyo imeandika kuwa Jay alikubaliana na promoter huyo aitwaye Eljah Ngirimani wa kampuni ya Black Slate ya mjini Mombasa kuhusu show 2 ambazo zilikuwa tarehe 24 December iliyofanyika Jambori na Tarehe 25 Iliyofanyika Kwetu Beach. Show zote Prof Jay alizifanya kama ilivyopangwa ila ulipofika muda wa kulipwa ndio matatizo yalianza.
Amesema promoter huyo alishindwa kumlipa pesa alizotakiwa kumlipa na kwa sasa bado promoter huyo anadaiwa na Prof Jay shilingi 120,000 za Kenya ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 2 za Tanzania.Amedai kila akipigiwa simu promoter huyo alikuwa akimwahidi Jay kumlipa baadae lakini hakufanya hivyo.
Mchawi huyo wa rhymes amesema promoter huyo hakulipa hata nauli yake ya kurudi Tanzania na Ilibidi ajilipie nauli mwenyewe na watu wake na ndio maana aliondoka kabla ya kufanya show ya tarehe 31 December mjini Mombasa.Jay amesema ameshtushwa na taarifa hizi kwani yeye ndiye anadai na sio kudaiwa chochote na anaamini promoter huyo ameamua kuongea uongo kwenye vyombo vya habari ili kulinda jina lake.
Promoter huyo aliliiambia gazeti la The Star kuwa Profesa Jay hakuwa amelipwa fedha zote kwa show ya pili na hivyo alipewa camera aina ya Nikon D3000 kama rehani.Baada ya show, Prof aliondoka nchini Kenya na crew yake na kuibeba kamera hiyo.
Issue hiyo imekuwa kubwa kiasi ambacho passport ya mpambe aliyekuwa amesafiri na Jay nchini humo imeshikiliwa ili asiondoke.Waandaaji wanadai kuwa walimlipa Profesa Jay shilingi 252,000 za Kenya ambazo ni zaidi hata ya fedha walizokuwa wamekubaliana na sasa wanataka warudishiwe fedha yao.
.
Featured Post
NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne ambayo ni Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...






