MASHAUZI CLASSIC BAND WAJIPANGA KULITEKA SOKO KWA UJIO WA ALBAM YAO MPYA
JAMII 3:22 PM
MSANII wa taarabu ambaye ni mmiliki wa bendi ya ‘Mashauzi Classic’, Isha Mashauzi, amesema kuwa wanajipaga kutoa albamu yao inayokwenda kwa jina la ‘Si bule una mapugufu’, ambayo itakuwa na nyimbo nne huku ikitarajia kuwa sokoni Aprili mwaka huu.
Alizitaja nyimbo hizo kuwa ni ‘Si bule una mapungufu’, ‘Niacheni nimpende’, ‘Fungu la kukosa’, ‘La mungu halina muamuzi’.
Isha alisema albamu hiyo ndiyo itakayo mtambulisha yenye pamoja na bendi yake kwani anaamini itafanya vizuri kuliko nyimbo zile ambazo alikuwa anaziimba awali.
“Hiyo ndo mpya ambayo tunayo hivi sasa na tunaamini albamu hiyo itakuwa moto wa kuotea mbali kwani nyimbo zote zimetungwa kwa umakini wa hali ya juu,” alisema.
Aliongeza kuwa anawashauri mashabiki wa muziki wataarabu hasa wapenzi wa Mashauzi Classic nchini kukaa tayari kuipokea albamu hiyo kwani uzinduzi wake utakuwa baada ya kutoka ambapo ni mwezi wa nne.
Alizitaja nyimbo hizo kuwa ni ‘Si bule una mapungufu’, ‘Niacheni nimpende’, ‘Fungu la kukosa’, ‘La mungu halina muamuzi’.
Isha alisema albamu hiyo ndiyo itakayo mtambulisha yenye pamoja na bendi yake kwani anaamini itafanya vizuri kuliko nyimbo zile ambazo alikuwa anaziimba awali.
“Hiyo ndo mpya ambayo tunayo hivi sasa na tunaamini albamu hiyo itakuwa moto wa kuotea mbali kwani nyimbo zote zimetungwa kwa umakini wa hali ya juu,” alisema.
Aliongeza kuwa anawashauri mashabiki wa muziki wataarabu hasa wapenzi wa Mashauzi Classic nchini kukaa tayari kuipokea albamu hiyo kwani uzinduzi wake utakuwa baada ya kutoka ambapo ni mwezi wa nne.






