UJAZO WA MAJI KATIKA BWAWA LA KIDATU WAONGEZEKA



 Msimamizi wa zamu wa Idara ya kuendesha mitambo ya kufua umeme katika mgodi wa Kidatu kwa kutumia kompyuta , Joseph Mwansasu ( wapili kutoka kulia) akimuonesha Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam Malima ( wa kwanza kulia) mfumo wa Teknolojia ya Kompyuta za kuwasha mashine nne za kufua umeme kwenye mgodi wa Kidatu kilingana na mahitaji ya Umeme nchini , Naibu Waziri huyo aliutembelea Mgodi huo Januari 8, mwaka huu, ili kuona hali halisi ya uzalishaji wa umeme na kiwango cha maji kwenye  Bwawa la Kidatu.
 Kaimu Maneja wa Mgodi wa Kidatu , Joseph Lyaruu , ( mwenye tochi) akimuonesha Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam Malima ( wa kwanza kulia) kifaa kilichobadirishwa baada ya kufanya kazi muda mrefu na kufanya sehemu nyingi kusagika na maji  wakati wa kuzungusha  mtambo wa kufua umeme ndani ya mgodi wa Kidatu, Naibu Waziri huyo aliutembelea Mgodi huo Januari 8, mwaka huu ,  ili kuona hali halisi ya uzalishaji wa umeme na kiwango cha maji kwenye  Bwawa la Kidatu.


Bwawa la Kidatu likoonekana kuanza kujaa maji ya mvua baada ya kunyesha mvua za kutoka katika Mikoa ya Iringa, Mbeya, Singida na Morogoro , ambapo hadi kufikia Januari 8, mwaka huu ujazo ulifikia mita 690.5 kutoka 680 ambalo ni ongozeko la mita 10.5 kwa muda wa miezi mitatu ya mvua zilizonyesha

Posted by Bigie on 12:14 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.