“MWANANGU”-SAJNA Feat.VUMILIA



Wimbo huu ulinifikia wiki kadhaa zilizopita.Kwa bahati mbaya na kwa sababu ambazo kwa kiasi kikubwa zilikuwa nje ya uwezo wangu,sikupata muda wa kuusikiliza kwa makini na kisha kukupa wewe msomaji na mfuatiliaji wa Mpekuzi  nafasi ya kuusikiliza. 

Kwa kifupi,si kila wimbo unaotumwa hapa huwa unawekwa moja kwa moja.Hapana.Kuna viwango na kuna utaratibu.

Lazima usikilizwe,wakati mwingine zaidi ya mara tatu na watu tofauti.Ukipita basi huwekwa hewani.Nia ni kusaidia watu watunge nyimbo za maana zaidi kwa maana ya ujumbe na producers waumize vichwa zaidi.

Basi leo muda umepatikana na naomba nikuletee kitu toka kwa Tetemesha Records kutoka kwa msanii wao,Sajna akiwa amemshirikisha msanii mwingine anayekwenda kwa jina Vumilia. Wimbo unaitwa Mwanangu

Huu ni wimbo ambao unazungumzia mapenzi ya mzazi kwa mwanae, na umelenga pande zote yaani mzazi wa kike na mzazi wa kiume, pia mtoto wa kike na mtoto wa kiume. 

Lakini pia hata wale ambao hawajapata watoto hawakusahaulika. 

Hivyo kwa mantiki hii ni wimbo unaomgusa kila mmoja katika jamii. Usikilize hapa chini na chini tena unaweza kusoma Lyrics za wimbo huo.




Song details

Track Name: MWANANGU
Artists: SAJNA ft. VUMILIA
Lyrics composed by: SAJNA, JOSEFLY & KID BWOY
Arranged by: KID BWOY
Produced by: KID BWOY & AMBA


Mixed by: KID BWOY
Studio: TETEMESHA RECORDZ
April 2012



“MWANANGU” Lyrics by SAJNA ft. VUMILIA


Track Name: MWANANGU
Artists: SAJNA ft. VUMILIA


Lyrics composed by: SAJNA, JOSEFLY & KID BWOY
Arranged by: KID BWOY
Produced by: KID BWOY & AMBA
Mixed by: KID BWOY
Studio: TETEMESHA RECORDZ
April 2012




Intro:

Mmmmmmh mmh, eeeeh eeh

Oooouuh oooh uuuuh oooh



Chorus
Sijaona kitu kizuri hapa duniani, kama mwanangu,
Yeye damu yangu, mimi baba yake,


Napopata kitu kidogo kikubwa, nakula na mwanangu,
Yeye damu yangu, mimi baba yake,

Verse 1:

Leo watasema madogo, kesho watazua makubwa,
Ujana maji ya moto, umepoa kwa huyu mtoto,
Kweli uanaume ni joto, pale unapokosa mtoto,
Wengi wametenga wake zao kwa kukosa mtoto,
Ufanisi wa jiko ni moto, furaha ya ndoa mtoto,


Nashangaa dada zangu wanaoamua bila hiyana kutupa watoto,
Mtoto wa udongo haoshwi, wa plastiki moto haoti,
Umepewa wa bin-Adam huna budi kusema Asante.

Chorus:
Sijaona kitu kizuri hapa duniani, kama mwanangu,
Yeye damu yangu, mimi baba yake,
Napopata kitu kidogo kikubwa, nakula na mwanangu,
Yeye damu yangu, mimi baba yake,



Verse 2:
Mwanangu kua kua nikutume, ufike kwa mfalme,
Uende kutetea wanyonge, ugumu wa maisha ukome,
Mshike elimu usimuachie,tamaa ujinga zikache,
Wanasema wa mwenzio ni wako, na wewe wangu ni wao,
Kila mmoja mpe heshima, awe na mali asiwe na mali,
Mpe heshimaaa, mpe heshima wewee.

Chorus


Sijaona kitu kizuri hapa duniani, kama mwanangu,
Yeye damu yangu, mimi baba yake,
Napopata kitu kidogo kikubwa, nakula na mwanangu,
Yeye damu yangu, mimi baba yake,

 Verse 3:
Ni zawadi ya pekee, niliyopewa mieee,
Ni mtoto wa kike acheni mi niringee,
Aliomnyima ndege utashi na kumpa mbawa arukee,


Ndie aliyenipa mie, mtoto huyu wa kike..
Amenitendea haki nyumbani furaha telee,
Ni mwenyezi Mungu milele ashukuriwe

Bridge
Usikate tamaa, omba na wewe eeeh,
Mungu ni mwema hatoacha chozi lipoteee,
Usivunjike moyo, omba na wewe eeeh
Tena na tena ilimradi usichokeee



Usitupe mtoto  si kosa lake yeye,
Mpe malezi bora na elimu aringe baadae,
Alokupa ni mwema wengi wamtafuta yeye,
Uzae japo mmoja ili ndoa itulie.

Bridge
Usikate tamaa, omba na wewe eeeh,
Mungu ni mwema hatoacha chozi lipoteee,


Usivunjike moyo, omba na wewe eeeh
Tena na tena ilimradi usichokeee

Chorus
Sijaona kitu kizuri hapa duniani, kama mwanangu,
Yeye damu yangu, mimi baba yake,
Napopata kitu kidogo kikubwa, nakula na mwanangu,
Yeye damu yangu, mimi baba yake,

 Outro


Mwanangu, we mwanangu
Mwanangu, we jembe langu
Mwanangu, we mwanangu,
Mwanangu, wewe jembe langu x2

Oooh oh, Tetemesha
Tete Tetemesha, bwoy bwoy bwoy bwoooooy

Sajna Saj, Sajnaaaaa




End

Posted by Bigie on 7:24 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.