MWIMBAJI AMINI ATAJA IDADI YA WASICHANA ALIO WAHI KUWA NAO


Mwimbaji AMINI ambae juzi ametoa video ya single yake mpya ya NI WEWE ameweka wazi  upande wake mwingine wa mapenzi sasa hivi baada ya kuachana na LINAH mwaka jana.

Amini amesema “Ilinichukua miezi kama kumi kukaa bila kuwa na mpenzi ambapo mwezi wa kumi na moja ndio nikapata mpenzi mpya, na mpaka sasa uhusiano wangu mpya una miezi michache”

 Amini amefunguka zaidi  kwamba katika dunia yake ya mapenzi, mwimbaji LINAH SANGA ndio alikua msichana wake wa kwanza, na huyu alienae sasa hivi ni wa pili.

Alipoulizwa kama kupitia kwenye relationships nyingi kuna mfanya aandike vizuri mashairi, Amini alikuwa na haya:

 “hapana, naandika nyimbo nzuri kutokana na kipaji changu, marafiki ninao ishi nao pamoja na mafunzo niliyopata THT, kwa hiyo sio mapenzi yanayonifanya niandike nyimbo nzuri”

Posted by Bigie on 6:19 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.