SURA MPYA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI
JAMII 6:29 AM
Sura mpya zitatawala Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uteuzi mpya, unaotarajiwa kufanywa wakati wowote na Rais Jakaya Kikwete, imebainishwa.
Vyanzo vyetu vimesema kuwa baada ya mtikisiko mkubwa uliotokea bungeni kwa wabunge kutaka kuisulubu serikali, sura mpya zinaingizwa ili kurejesha imani ya mihimili hiyo miwili.
Vimebainisha kuwa iwe mawaziri wanane waliochafua hali ya hewa, kutoswa na kujaza nafasi zao au baraza la mawaziri kuvunjwa na kuundwa jipya, sura mpya zitatawala.
Imeelezwa kuwa katika sura hizo mpya, vijana wanapewa kipaumbele na tayari majina yao yameshaanza kupenyezwa ili wapewe kipaumbele kwa lengo la kuleta nguvu mpya, hivyo kurejesha imani kwa wananchi juu ya serikali yao.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Harrison Mwakyembe, anapigiwa chapuo la kupandishwa daraja kutoka unaibu na kuwa waziri kamili kwa sababu anajitosheleza.
Sura za vijana ambao wanapendekezwa kupewa nafasi za kuongoza wizara ni Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba, Peter Serukamba (Kigoma Mjini) na George Simbachawene (Kibakwe).
Vijana wengine ni Faustine Ndugulile (Kigamboni), Said Mkumba (Sikonge) na Vita Kawawa (Namtumbo).
Katika chapuo hilo, wanawake wanaotajwa kwamba awamu hii wataula ni Jenister Mhagama (Peramiho), Zainab Kawawa (viti maalum) na Injinia Stella Manyanya (viti maalum).
Wengine wanaotarajiwa kwa tumaini kubwa ni Mbunge wa Serengeti, Steven Kebwe na Festus Limbu wa Jimbo la Magu.
Aidha, habari zinasema kuwa endapo baraza litavunjwa, kuna manaibu wengi watakwenda na maji.
Kati ya manaibu ambao hali zao ni mbaya ni Lazaro Nyalandu (Viwanda na Biashara), Athuman Mfutakamba (Uchukuzi), Adam Malima (Nishati na Madini) na Lucy Nkya (Afya).
Kwa sasa kaa la moto lipo kwa mawaziri Mustafa Mkulo (Fedha na Uchumi), George Mkuchika (Tamisemi), Ezekiel Maige (Utalii), Jumanne Maghembe (Kilimo, Chakula na Ushirika), Cyril Chami (Viwanda na Biashara), Omar Nundu (Uchukuzi) na Haji Mponda (Afya).
Vyanzo vyetu vimesema kuwa baada ya mtikisiko mkubwa uliotokea bungeni kwa wabunge kutaka kuisulubu serikali, sura mpya zinaingizwa ili kurejesha imani ya mihimili hiyo miwili.
Vimebainisha kuwa iwe mawaziri wanane waliochafua hali ya hewa, kutoswa na kujaza nafasi zao au baraza la mawaziri kuvunjwa na kuundwa jipya, sura mpya zitatawala.
Imeelezwa kuwa katika sura hizo mpya, vijana wanapewa kipaumbele na tayari majina yao yameshaanza kupenyezwa ili wapewe kipaumbele kwa lengo la kuleta nguvu mpya, hivyo kurejesha imani kwa wananchi juu ya serikali yao.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Harrison Mwakyembe, anapigiwa chapuo la kupandishwa daraja kutoka unaibu na kuwa waziri kamili kwa sababu anajitosheleza.
Sura za vijana ambao wanapendekezwa kupewa nafasi za kuongoza wizara ni Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba, Peter Serukamba (Kigoma Mjini) na George Simbachawene (Kibakwe).
Vijana wengine ni Faustine Ndugulile (Kigamboni), Said Mkumba (Sikonge) na Vita Kawawa (Namtumbo).
Katika chapuo hilo, wanawake wanaotajwa kwamba awamu hii wataula ni Jenister Mhagama (Peramiho), Zainab Kawawa (viti maalum) na Injinia Stella Manyanya (viti maalum).
Wengine wanaotarajiwa kwa tumaini kubwa ni Mbunge wa Serengeti, Steven Kebwe na Festus Limbu wa Jimbo la Magu.
Aidha, habari zinasema kuwa endapo baraza litavunjwa, kuna manaibu wengi watakwenda na maji.
Kati ya manaibu ambao hali zao ni mbaya ni Lazaro Nyalandu (Viwanda na Biashara), Athuman Mfutakamba (Uchukuzi), Adam Malima (Nishati na Madini) na Lucy Nkya (Afya).
Kwa sasa kaa la moto lipo kwa mawaziri Mustafa Mkulo (Fedha na Uchumi), George Mkuchika (Tamisemi), Ezekiel Maige (Utalii), Jumanne Maghembe (Kilimo, Chakula na Ushirika), Cyril Chami (Viwanda na Biashara), Omar Nundu (Uchukuzi) na Haji Mponda (Afya).





