JWTZ WAONGEZA NGUVU BAADA YA MAHARAMIA KUWAZIDI POLISI NGUVU KIGOMA.
JAMII 6:08 PM
Kigoma.Mwandishi Emmanuel Johnson amesema “baada ya polisi kwenda mapambano yalikua magumu hivyo wakarudi kuomba msaada JWTZ ambapo tangu asubuhi walijibizana kwa risasi na maharamia na kupelekea wanajeshi watatu na polisi wawili kujeruhiwa kwa risasi”
Majeruhi wamelazwa kwenye chumba cha upasuaji ndani ya hospitali ya mkoa ya Maweni na mpaka sasa hakuna taarifa rasmi kutoka kwenye vyombo vya usalama lakini imeahidiwa kwamba May 3 2012 ndio watatoa taarifa japo hali ya usalama imeripotiwa kuwa nzuri baada ya maharamia kupigwa na kuzamishwa baada ya jitihada za kuwakamata kushindikana.
Tutazidi kukupa kinachoendelea.





