MKANGANYIKO WA LEO: JAMES OLE MILLYA (CHADEMA ) SIYO MKUU WA WLAYA


Mpekuzi,
Napenda kutoa ufafanuzi kuhusu mkuu wa wilaya ya Longido James Ole Millya kama ifuatavyo.. 

James Ole Millya wa CHADEMA siyo mkuu wa wilaya kama wengi wanavyodhani ila ukweli ni kuwa wakati James anazaliwa alipewa jina la mjomba wake aitwaye James Ole Millya ambaye ni ndiye mkuu wa wilaya ya Longido na wala siyo kuwa aliteuliwa juzi bali hata kabla ya uteuzi ule still alikuwa mkuu wa wilaya ile ile. 
 
Kwa hiyo JAMES OLE MILLYA CHADEMA (kijana) alirithishwa jina la kaka wa mama yake tumuite JAMES OLE MILLYA CCM (mtu mzima) ambaye ndiye DC wa Longido mkoani Arusha. Sometimes ni tamaduni za kimasai tu kurithishana majina. 
 
Asiyeelewa arudie kusoma taratibu then kama hajaelewa aulize tu. 
 
Naomba kutoa hoja.

Mjumbe, Arusha.

Posted by Bigie on 1:42 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.