MKUU WA MKOA WA IRINGA AVURUGA UCHAGUZI WA SERIKALI YA WANAFUNZI- CHUO KIKUU CHA RUAHA ( RUCO )
JAMI 6:31 PM
Akizungumza na Mpekuzi wetu ,Spika wa Bunge la wanafunzi Sinkala Luka amesema wameshangazwa na uamuzi huo wa Ishengoma na kudai kuwa hatua hiyo ni ya vurugu na inayokiuka taratibu na kanuni za chuo.
Luka alidai kuwa mkuu huyo wa mkoa, mbali na kusitisha uchaguzi huo, ameamuru viongozi wa tume ya uchaguzi walioapishwa kwa ajili ya kusimamia kujiuzulu bila sababu za msingi.
“Kwa ujumla tunashangazwa sana na kitendo cha mkuu wa mkoa kuacha majuku yake kwa jamii na kujiingiza katika uchaguzi wa serikali yetu ambao hauingiliani kabisa na majukumu yake, na huu ni uvunjifu wa taratibu kwa kuwa kamwe sisi wanafunzi hatujawahi kumuingilia yeye katika nafasi yake.
Kwa mujibu wa katiba ya serikali ya wanafunzi chuoni hapo, ofisi ya spika inapewa mamlaka ya kuteua majina ya wagombea kutoka kila kitivo kulingana na uhitaji wa majina hayo.
Mwandishi wetu alipomtafuta mkuu wa mkoa kwa ajili ya kutoa ufafanuzi juu ya suala hilo, juhudi ziligonga mwamba kwa kile kilichoelezwa na mhusika wa mapokezi kuwa mkuu huyo hana nafasi ya kuonana na mtu yeyote. Hata alipopigiwa simu ya mezani pamoja na ya mkononi hazikupokelewa.
Mbunge wa Iringa mjini Peter Msigwa amesikitishwa na kitendo cha mkuu wa mkoa huyo kuingilia masuala ya wanafunzi badala ya kufanya kazi alizotumwa kwa jamii.
“Mimi namshauri mkuu wa mkoa aache kujidhalilisha kwa kuwa yeye ana nafasi yake ambayo anatakiwa kuwajibika kwa jamii. Tuwaache wanafunzi wawajibike kwa nafasi zao, tusiwaingilie maana wana miongozo yao na tujiepushe na aibu za kipuuzi,” alisemaMsigwa.
Kumekuwa na tuhuma nzito kuwa baadhi ya viongozi wa siasa wakishinikizwa na mfanyabiashara mmoja maarufu na mwanachama wa Chama cha Mapinduzi, kuhakikisha kuwa watakaochaguliwa ni wale tu walio wanachama wa CCM.





