ODAMA: NAKULA ‘BATA’ KWANZA, NDOA BAADAYE



MWANADADA anayefanya vizuri kunako gemu la filamu Bongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’ amefunguka kuwa kwa sasa hawezi kukurupukia kuolewa hadi atosheke kula starehe ‘bata’ kwa kujinafasi.

Akichonga na paparazi wetu, Odama alisema amefikia hatua ya kusema hivyo kwa kuwa, anajua ndoa inahitaji utulivu kiasi kwamba akiolewa haraka huku akiwa bado ana hamu ya kujiachia anaweza kutibua ndoa.


“Ukiwa ndani ya ndoa utakuwa unabanwabanwa na mwanaume, huwezi kula bata kama unavyoweza kula ukiwa singo kwa hiyo bora nimalizie kabisa nikiingia huko niwe nimetosheka,” alisema Odama.


Akaongeza kuwa, wengi ambao ndoa zao hazidumu wamepapatikia kuolewa ila yeye ataolewa akiwa na miaka 35 na atazaa mtoto mmoja tu.

Posted by Bigie on 1:29 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.