SEAN KINGSTON AFUNGULIWA KESI NA BABA MWENYE NYUMBA!

Msanii Sean Kingston yupo matatani.Kwanini? Ni hivi, aliyekuwa mwenye nyumba wake wa huko Miami,Florida, amefungua kesi akidai kwamba msanii huyo amesababisha uharibifu mkubwa katika nyumba aliyokuwa akipanga kwa kiasi cha dola $25,000 kwa mwezi na pia amevunja mkataba wa upangaji.

Sean Kingston ambaye ni miongoni mwa wasanii kutoka US waliowahi kutua Tanzania anadaiwa kwamba yeye na mama yake walipanga nyumba hiyo tangu October mwaka jana kabla ya kuamua kuondoka tu ghafla mwaka huu kabla mkataba haujaisha. Mwenye nyumba anasema licha ya kuondoka ghafla, wapangaji wake hao wametia hasara ya $21,397 kutokana na kuharibu samani zilizopo katika nyumba hiyo.

Mwenye nyumba huyo pia anasema Sean Kingston na mama yake hawakulipa kodi ya pango kwa miezi miwili ya mwisho na hivyo anawataka walipe kiasi cha $73,816.85 ikiwa ni pango pamoja na riba.

Kwa mujibu wa tovuti ya TMZ, mpaka hivi sasa kambi ya Sean Kingston haijasema chochote kuhusiana na kesi hiyo.

Bila shaka unaweza kujiuliza,inakuwaje msanii kama Sean Kingston, asiwe na nyumba yake mwenyewe kiasi kwamba awe mpangaji mpaka leo? Well…sijui lakini kumbuka hata Michael Jackson alifia kwenye nyumba ya kupanga!

Posted by Bigie on 9:07 PM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.