"ADUI SIO MTU WA KUMSAHAU HATA KAMA HUNA KINYONGO NAYE"...LORD EYEZ

Kwenye exclusive interview na Clouds fm, rapper kutoka A City Lord Eyes amefungua mengine kutoka moyoni mwake kuhusu fitna zinazofanywa dhidi yake.

 ” Hata mambo yanavyoenda nafikiri wewe mwenyewe unaona na kuna vitu pia nimeviona na kuna watu pia nimewaona, unajua adui sio mtu wa kumsahau hata kama hauna kinyongo nae lakini usimsahau kwamba ni adui”LORD EYEZ

Baada ya kuyasema hayo Lord Eyes ambae yuko nje kwa dhamana baada ya kushikiliwa na polisi kwa zaidi ya siku 10 kutokana na tuhuma za wizi wa vifaa vya gari la msanii Ommy Dimpoz hakutaka kuendelea tena kuzungumza ila hiyo ndio msg fupi aliyotaka kuizungumza.

Mpaka sasa amesema ni nyimbo tatu alizonazo kichwani zenye mistari kuhusu kilichomkuta kwenye tuhuma hizo za wizi ambazo atazitoa na kuna uwezekano moja akaitoa december hii.

Posted by Bigie on 12:38 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.