JIHADHARI NA WEZI WANAOCHANGISHA FEDHA ZA MSIBA WA SAJUKI




Kwa mujibu wa Steve Nyerere ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya mazishi ya marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’ aliyefariki dunia jana, kumejitokeza watu wanaojifanya kutumwa na familia kuchangisha fedha kwa njia ya simu.


Steve amesema kuna mtu mmoja anayetumia jina kubuni Tumaini ameendelea kukusanya fedha nyingi kutoka kwa watu mbalimbali na kusema kuwa waache mara moja kwakuwa ni mwizi.

Steve amekielezea kitendo hicho kama wizi usio na aibu kwa familia ya Sajuki iliyopo kwenye majonzi makubwa.

Ameongeza kuwa taratibu zote za kukusanya fedha zinaendelea msibani maeneo ya Tabata jijini Dar es Salaam huku yeye na Mike Sango wakihusika na ukusanyaji huo.

Posted by Bigie on 2:52 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.