PICHA ZINAZOONYESHA TATTOO MPYA YA MSANII RAYUU PAMOJA NA NGUO ZA NDANI ZASAMBAA TENA

WAKATI wadau wa tasnia ya filamu wakitarajia kuona tasnia hiyo ikiwa imebadilika hali bado tete, ambapo msanii ‘Rayuu’, ameanza vituko kwa kuonesha tattoo yake mpya huku akiwa kwenye pozi tata ambalo linamuonesha hadi nguo yake ya ndani.

Msanii huyo mwaka uliopita aliandamwa na skendo ya kutembea na mwanaume wa mtu pamoja na ishu kadhaa, lakini mbali na haya bado mwaka huu anaonekana kuwa moto wa kuotea mbali.


Mwandishi wetu alifanya mchakato wa kumtafuta ili kuzungumza naye juu ya ujio huo ambao unaweza kuleta maneno mtaani, ambapo alidai kuwa hakuna mtu anayeweza kumzuia katika jambo analotaka kulifanya.


Alisema kuwa picha hiyo haimanishi kwamba anavunja maadili ingawa baadhi ya watu wanaamini hivyo, pale wanapoona tattoo ama nguo ya ndani.


“Ni kweli nimepiga picha ambayo inanionesha sehemu kubwa ya kiuno changu pamoja na nguo yangu ya ndani lakini halimanishi kwamba mimi ni muhuni au navuja maandili hapana ni kitu kidogo sasa ningevua nguo kabisa ingekuaje,” alidai msanii huyo bila haya.

Posted by Bigie on 9:52 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.