"MAPENZI YAMENIPOTEZEA MUDA NA KUNIFANYA NUJUTE"....NISHA


STAA wa la filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ amefunguka kuwa anajuta kupoteza muda mwingi kwenye mapenzi kuliko kazi mwaka jana.

Akiongea na mwandishi wetu, Nisha alisema amebaini kuwa mwaka 2012 mapenzi yalimfanya ashindwe kutimiza malengo yake mengi kwenye soko la filamu.


“Mwaka jana nilipelekwa puta sana na mapenzi. Mara kigogo, Geofrey na Nay wa Mitego jambo ambalo lilinifanya nishindwe kufanya kazi kwa ufanisi. Mwaka huu sikubali, mwendo wa kazi tu siyo mapenzi,” alisema Nisha.


Aidha, aliongeza kuwa atahakikisha anashirikiana vizuri na wenzake katika kazi zake.

Posted by Bigie on 10:09 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.