HUYU NDO MSANII ALIYEFUKUZWA KUTOKANA NA U-HANDSOME ULIOPITILIZA


Huyu ni Omar Borkan Al Gala, mwigizaji na pia mpiga picha wa huko Dubai ambaye kwa mujibu wa taarifa, yeye pamoja na wenzake wawili wamefukuzwa huko Saudi Arabia kutokana na kuwa na muonekano mzuri kupitiliza
(Yaani ma-handsome kupita kiasi) ili kuepusha kuwaingiza katika tamaa wanawake ambao hushindwa kujizuia kuwashobokea.

Omar alitolewa na maafisa wa polisi na kunyimwa kuhudhuria katika tamasha ambalo hufanyika kila mwaka nchini humo ambalo huusisha mbio za Ngamia, Janadriyah Festival ambalo kwa sehemu kubwa huhudhuriwa na matajiri, na baadhi ya vyanzo vya taarifa vinasema Omar alitolewa kutokana na mualiko wa msanii wa kike maarufu kutoka Falme za Kiarabu ambaye walihofia angeweza kutengeneza mahusiano naye.... na wengine wakisema ni hofu ya wakubwa kuibiwa mademu wao.

Posted by Bigie on 1:30 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.