FIFA YAWARUDISHA MALINZI NA WAMBURA KUGOMBEA TFF

Kuna taarifa kwamba wagombea wawili, Jamal Malinzi na Michael Wambura wamerudishwa kuwania nafasi walizokuwa wakipigania kuzipata katika uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Taarifa kutoka ndani ya TFF zimeeleza, Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limeandika barua ambayo imeshatua Fifa tayari kuwarejesha Malinzi, Wambura na wengine waliokuwa wanagombea.

Uongozi wa TFF unatarajia kuzungumza muda mfupi ujao kuanzia sasa katika ofisi zake katika eneo la Ilala jijini Dar es Salaam.

Tayari Salehjembe ametega masikio kuhusiana na kitakachotokea na atatutaarifu kama ni hiki kutoka ndani au kutakuwa na mabadiliko.

Posted by Bigie on 5:14 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.