"SIJAWAHI MVULIA NGUO MWANA FA"...HUSNA



MISS Sinza 2011, Husna Maulid, juzikati ameibuka na kudai kwamba katika maisha yake hajawahi kutoa penzi kwa msanii wa muziki wa Kizazi Kipya, Hamis Mwijuma ‘Mwana FA’.

Husna aliyasema hayo Mei 15 mwaka huu baada ya kuvumishiwa kuwa anatoka kimapenzi na staa huyo na kwamba, kwa sasa hakuna kificho chochote kwani hadi picha zinazowaonyesha ukaribu wao zimezagaa kwenye mtandao.


“Sijawahi kutoka na Mwana FA, zaidi ya kufanya naye tangazo ambalo niliombwa na dada’ngu, Mboni Masimba nikafanye naye kwa ajili ya shoo ambayo anaiandaa hivi karibuni, wanaonihusisha na mapenzi na Mwana FA hawanitendei haki hata kidogo maana sijawahi hata kuwa na wazo naye,” alisema Husna Maulid.

Posted by Bigie on 1:38 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.