UKUMBUSHO: TAREHE KAMA YA LEO, RAIS NELSON MANDELA ALIFUNGWA MIAKA 27 JELA

Siku kama ya leo (June 12) mwaka 1964 viongozi wapatao 8 wa chama cha ANC akiwemo rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela walihukumiwa kwenda jela, ambako mzee Mandela alitumikia kifungo kwa miaka 27.

Mzee Madiba ambaye leo anafikisha siku ya 5 akiwa amelazwa hospitalini akisumbuliwa na mapafu huko Afrika Kusini, ndiye alikuwa rais wa kwanza mweusi kwa taifa hilo.


Kwa mujibu wa BBC Kwa sasa Afya ya Mandela bado si nzuri na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini anaendelea kuwaomba wananchi wa taifa hilo kuendelea kumuombea mzee Madiba aweze kupona.

Posted by Bigie on 4:33 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.