UPDATE: LWAKATARE AKWAMA KUPEWA DHAMANA TENA....HAKIMU ALIKUWA HAJAYAPITIA MAFAILI YAKE

Lwakatare (kulia) na mtuhumiwa mwenzake Ludovick wakiwa mahakamani leo.
 Baadhi ya wanachadema waliofika mahakamani leo.
Lwakatare akifunguliwa pingu.

Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Muganyizi Lwakatare, kwa mara nyingine ameshindwa kuwekewa dhamana leo katika kesi inayomkabili ya kujaribu kumwekea sumu Dennis Msaki iliyosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisuru jijini Dar es Salaam. 

Sababu za kuahirishwa kesi hiyo ni madai ya hakimu kuwa hakuweza kupata muda wa kupitia mafaili ya kesi hiyo maana alikuwa likizo. Lwakatare amerudishwa Segerea na kesi yake imetajwa kurudishwa mahakamani kesho asubuhi (Juni 11 mwaka huu).

Posted by Bigie on 4:07 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.