BEYONCE AUMBUKA BAADA YA NYWELE ZAKE KUNASWA NA FENI AKIWA KATIKA SHOW HUKO CANADA


Jumatatu usiku (July 22) Beyonce alikuwa na show huko Montreal, Canada...

Wakati anaimba wimbo wake wa ‘Hallo’ ghafla  nywele zake zikanaswa na feni iliyokuwa nyuma yake jukwaani hapo, nina uhakika kwa msanii mwingine angeweza hata kupoteza mwelekeo na huenda ingemharibia show..


Lakini uzoefu na kujiamini vilimsaidia Bey mama wa mtoto mmoja (Blue Ivy) ambaye hakutetereka na aliendelea kuimba bila hata kupoteza mstari wala kutoka nje ya beat (Ki professional zaidi). 


Bey alisimama kwa muda huku wasaidizi wake wakijaribu kukata sehemu ndogo ya nywele zake na mkasi ili aweze kuwa huru na kuendelea na show. Zoezi lilifanikiwa na kipenzi cha Jigga aliendeleza makamuzi.

Posted by Bigie on 5:11 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.