"NAOLEWA KWA AJILI YA STAREHE ZA MAPENZI NA SI KWA AJILI YA KUZAA"...NATASHA WA BONGO MOVIE


MWIGIZAJI mkongwe wa maigizo na filamu Bongo, Suzan Lewis ‘Natasha’ ambaye pia ni mtangazaji wa Radio Times FM, anayetarajia kufunga ndoa kesho, amefunguka kuwa anaoelewa kwa ajili ya kustarehe na siyo kwenda kuzaa kama wengine wanavyofanya.

Akizungumza na mwandishi wetu, Natasha alisema kuwa katika maisha yake hakuna kitu anachokichukia kama kubeba mimba na umri alionao ndiyo kabisa hawezi kufanya hivyo bali atalea wajukuu tu.
 

“Kuolewa si lazima kuzaa, mimi nimeolewa kwa ajili ya ‘ku-relax’ na kufurahi maisha kwa mume wangu na si vinginevyo, wakati wa kuzaa umeshapita, namwachia Monalisa (mwanaye) sasa aendelee kuijaza dunia,” alisema Natasha.

Mwanamama huyo ambaye hivi karibuni alifanyiwa bonge la pati katika sherehe ya kuagwa ‘send-off’ katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar alisema kuwa anaiombea ndoa yake idumu miaka mingi, wafe wazikane.

Posted by Bigie on 12:51 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.