MSANII SHETTA AMALIZA BIFU NA BABA YAKE BAADA YA KUZINGUANA TANGU AKIWA NA MIAKA 7

 Baraka za mwezi Mtukufu wa Ramadhan zimeitembelea familia ya Baba Qayllah, Shetta Bilal. Baada ya miaka mingi ya maelewano hafifu na baba yake mzazi, leo baba na mwanae wameamua  kusameheana

Kupitia Instagram, Shetta amepost picha (hiyo juu) akiwa na baba yake mzazi Mzee Bilal ambaye ni Sheikh, pamoja na mdogo wake Awab na kuandika: Wit my daddy n my young broda Awab….. #happyday baada ya miaka mingi kuwa na tofauti na mzee tangu nina miaka 7 leo yameisha #bassawa #Ramadankareem.”

Mwandishi wetu amezungumza kwa simu na Shetta kutaka kupata maelezo zaidi ya kwanini alikuwa haelewani na baba yake.
“Basi tu tulikuwa tunakosana, nahisi situations zangu na maisha yangu vilikuwa haviko sawa. Kazi yangu ninayofanya na nini kwasababu yeye ni mtu wa dini sana, baba yangu ni Al Haj, Sheikh. Kwahiyo nahisi hilo lilikuwa tatizo kwa upande wake..”


Shetta amesema kwa muda wote huo baba yake alikuwa hamfahamu mke wake pamoja mwanae, Qayllah lakini sasa anafuraha kwakuwa wameyamaliza baba  yake amemuelewa.

Posted by Bigie on 8:40 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.