SHILOLE ATINGA DUKANI HUKO MAREKANI AKIWA NA TAULO TU...

MSANII wa filamu na muziki Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ametoa kali ya mwaka baada ya kunaswa akiingia ‘supermarket’ akiwa ametinga taulo.

Tukio hilo lilitokea hivi karibuni katika mji wa Maryland nchini Marekani ambapo staa huyo amekwenda kwa ajili ya kufanya shoo kisha kupigwa picha hiyo na rafiki yake ambaye aliiweka mtandaoni ikimuonesha akiwa amefunga taulo kwenye matiti.
 

Mwandishi wetu alipomuuliza Shilole kulikoni kupitia mtandao wa Instagram, alifunguka:
 

“Huku watu wanaishi kizungu hakuna mtu anayeshughulika na maisha ya mwenzake kila mmoja anahangaika na mambo yake kwa hiyo siyo ajabu mimi kuvaa taulo na kwenda nalo supermarket, huku ni kawaida tu.”

GPL

Posted by Bigie on 12:25 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.