Kufa kufaana: Polisi watumia nguvu kuwatawanya wananchi waliokuwa wakiiba mafuta baada ya lori kupinduka


Askari wa jeshi la polisi mkoa wa Morogoro wamelazimika kutumia nguvu  kuwatawanya wananchi  na kuwachapa viboko watu  waliokuwa wakiiba mafuta mara baada ya ajali la lori liliosheheni mafuta aina ya Dizel lililokua likitokea jinini Dar es Salaam kuelekea Zambia kupinduka katika eneo la Msamvu mjini Morogoro.

 ITV imeshuhudia baadhi ya wananchi wakiwa na ndoo na madumu huku kukiwa na mvutano  mkubwa  kati  yao  na  polisi ambapo wananchi hao  wametupia lawama askari wa jeshi la polisi kuwafukuza kwa madai  kuwa  hawaoni sababu kwani kuanguka kwa gari hiyo imekuwa ni fursa kwao.
 

Nae mkuu kituo cha usalama barabarani mkoa Morogoro wa Leonard Fungu akizungumzia tukio hilo amesema wamelazimika kutumia nguvu kuwatawanya wananchi waliokuwa wakiiba mafuta kwani wizi  wa mafuta kwenye matukio ya ajali si kitendo cha uungwana pia wanaweza kuhatarisha usalama wa maisha yao.


Ajali hiyo imetokea wakati  dereva wa lori alipokuwa akikata kona . Gari lilimshinda na kupinduka .

Posted by Bigie on 1:52 PM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.