Mayasa awashangaa wanaodai kuwa ameolewa.....Asema yeye yupo Single na hahitaji ndoa kwa sasa maana bado ni mdogo sana


Msanii  wa  kike  wa filamu Bongo, Mayasa Mrisho ( Maya ) amefunguka kuwa wale waliozusha kuwa amechumbiwa ni  wanafiki  na watasubiri sana   mpaka  wazeeke  kwani suala la ndoa kwake bado halipo leo wala kesho.

Akiongea na mpekuzi wetu, mrembo huyo  amedai kwamba uvumi ulionenezwa kuwa amechumbiwa ulikuwa una lengo la kumchafua   na  kumjaza  mikosi  ya  kupendwa  na  wanaume.

"Nawashangaa  wanaohangaika  kuumiza  midomo  yao  wakiwatangazia  watu  eti  nimechumbiwa. Mimi  nipo  single  na  sihitaji  kuolewa  kwa  sasa.

"Nahitaji  mpenzi  wa  kufarijiana  tu  maana  ndoa  ni  kifungo  ambacho  nadhani  sipo  tayari  kukitumikia  katika  umri  mdogo  kama  huu"



Posted by Bigie on 3:26 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.