Wanawake Acheni Vigenge Vya Umbeya Na Kuwa Magolikipa Kwa Wanaume: Happy Nyatawe


Muigizaji maarufu wa filamu nchini Happy Nyatawe ambaye pia ni mfanyabiashara amewaasa wanawake wenzake kuacha kuwa magolikipa kwa wanaume na pia kuacha umbeya na badala yake wajikite katika kazi ili kujiletea maendeleo.
 
Akizungumza na Mpekuaji, Happy  amesema:
"Nashangaa wanawake ambao mpaka karne hii wanategemea wanaume Kwanini siku moja na wewe mpenzi wako au mumeo asifurahie msaada toka kwako ?
 
"Wanawake tunaweza kataa u-golikipa na vikao vya umbeya mitaani, u-busy unaepusha mambo mengi sana .Tuwe  bize  kusaka  pesa  na  si  kusuta  watu.

"Mimi mbali na biashara yangu muda mwingi napenda kupumzika nyumbani na kuangalia movie, yaani kazi za wenzangu  na  endapo itatokea msiba au sherehe hujumuika na wenzangu lakini naogopa sana kusutwa ndo maana sipend vigenge"

Posted by Bigie on 5:38 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.