Wafuasi wa UKAWA Wavamia Msafara wa Magufuli Jijini Arusha Huku Wakiimba Lowassa!!!.....Lowassa!!........Mabomu Yarindima, 6 Watiwa Mbaroni

Mgombea  Urais  wa  Chama  cha  Mapinduzi  (CCM)  yuko  jijini  Arusha  ambapo  jioni  yupo  katikati  ya  jijini hilo  ndani  ya  uwanja  wa  Sheikh Amir Abeid,  akinadi  sera  za  chama  chake.

Kabla ya kufanya mkutano kwenye uwanja wa Sheikh Amir Abeid  jioni  hii, Dk. Magufuli alielekea kwanza wilayani Monduli leo asubuhi ambako alitafanya  kufanya  mkutano wa hadhara katika eneo la Mto wa Mbu  kwa  mujibu  wa  ratiba  yake.

Taarifa  tulizozipata  zinaarifu  kuwa  hali  haikuwa  nzuri  katika  eneo  hilo  la  Mto  wa  Mbu  baada  ya  msafara  wake  kukumbana  na wafuasi  wa  UKAWA  ambao  walivamia  msafara  huo  na  kuanza  kushangilia  wakisema  Lowassa!!!....Lowassa!!  Lowassa!!!  huku  wakiwa  wamenyoosha  vidole  viwili  juu.-Tazama  Video  Hii


Mkatafute pa humea hatuitaji pushap tunataka dawa mahospitali maisha bora na elimu bora
Posted by Pearsis Mwetha on Tuesday, October 6, 2015

Hali  hiyo  iliwafanya  polisi  waingile  kati  kwa  kupiga  mabomu  ya  machozi  ambapo  vijana  kadhaa wametiwa  mbaroni  wakituhumiwa  kuhujumu  mkutano  huo  wa  Magufuli.- Tazama  na Hii



Ccm arusha haina nafasii ni mda huu maandalizi ya magufuli ndo tunampokea namna hiii
Posted by Pearsis Mwetha on Tuesday, October 6, 2015
Mbali  na  matukio  hayo, Magufuli  amefanikiwa  kuliteka  jiji  la  Arusha  na  Watu  wamefurika  vya  kutosha  ndani  ya  uwanja  wa Sheikh Amir Abeid

Posted by Bigie on 6:57 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.