"NAJUTA KUWA NA H. BABA"....ASEMA FROLA MVUNGI


Staa  wa filamu, Flora Festo Mvungi, anateswa na mapenzi, hivi sasa anajuta kumpa penzi lake mwanamuziki Hamis Ramadhan Baba ‘H.Baba’.

Flora, aliyasema hayo  mbele ya mpekuzi  wetu wiki iliyopita kwamba kinachomfanya ajute kuwa na H. Baba ni namna H.Baba  anavyombana.


“Nabanwa sana na huyu mwanaume, yaani kila kona anataka niwe naye, sasa tunakuwa hatuwezi kufanya kazi za kimaendeleo, kila nikipokea simu, anataka ajue ni nani,” alisema Flora akifuta machozi na kuongeza:

“Hamis (H. Baba) ana wivu sana, ndiyo maana najuta kuwa naye.”


Msanii huyo ambaye alikutwa na mpekuzi  wetu akiwa amejiinamia, huku akitokwa na machozi, Kinondoni, alisema kuwa hivi sasa anakosa dili nyingi za kucheza filamu kwa sababu ya kubanwa na H. Baba.


“Kwa kweli inabidi niwe makini. Nisipokuwa mwangalifu nitazidi kufulia kwa huyu mwanaume. Nilichokuwa nakitarajia katika mapenzi kutoka kwake sicho ninachopata,” alisema.

Kutokana na hali hiyo, Flora alisema kuwa uamuzi wake kwa sasa ni kutafuta watu wenye busara wazungumze na H. Baba ili abadilike na kama asipoona mabadiliko, ataamua waachane.

Kutokana na malalamiko hayo, mpekuzi  wetu  alimtafuta  H. Baba ambaye alisema:
“Katika uhusiano wa kimapenzi au ndoa, kugombana ni suala la kawaida. Kumfuata Flora kila aendapo ni halali yangu maana ni mchumba wangu isipokuwa watu wanajaribu kuingiza maneno ili tutengane,” alisema H. Baba na kuongeza:

“Kama Flora alisema hayo basi zilikuwa ni hasira, maana kutofautiana kulitokea zamani na sasa tunaelewana vizuri. Haiwezi kutokea tena na wanaosubiri tuachane, basi watasubiri sana. Kama kuna makosa ya kibinadamu basi tutayamaliza,” alisema H. Baba 

Posted by Bigie on 1:00 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.