MUONEKANO WA JIJI LA DAR ES SALAAM MCHANA HUU BAADA YA MVUA YA JANA....
Posted by Bigie
JAMII
5:06 AM
Daraja la Luhanga limekatika na watu wanapita katika maji yenye kimo cha kiunoni Dar na foleni ya asubuhi.Hapa ni njia panda ya tabata segerea na foleni hii imeanzia Buguruni Godoro limenasa kwenye mti.Limeletwa hapo na maji jana Watu wakipata shida kutembea kwani maeneo mengi mitaani yamejaa maji Ukuta wa shule ya msingi Gonzaga Luhanga umebomolewa na maji jana Leo Ubungo maziwa.Maduka,bucha na saloon vikiwa vimefungwa na maji yamejaa ndani Mti mkubwa umeng'olewa na kuangukia nyumba hivyo kusababisha uharibifu mkubwa,Mabibo Familia zikihangaika kumalizia usafi katika nyumba zao.Samani hizi hasa masofa yameharibiwa kabisa Mabibo,nyumba zimeharibiwa na maji ya mto Kigogo mwisho, baadhi ya vitu vya familia ambazo bado hazijapata ufumbuzi juu ya makazi yao Mzee huyu anaendelea na usafi wa nyumba yake maeneo ya Luhanga Luhanga, hapa watu wamelala usiku wanapaita camp baada ya kuwa wameshindwa kumaliza kutoa tope katika nyumba zao Daraja la kigogo limekatika.vijana wameweka nguzo za umeme na wanatoza 500 kwa kila anayepita hapo.anayeogopa kuvuka mwenyewe wanamsaidia kuvuka kwa sh 1000. Hapa vijana wakimsaidia dada kuvuka Nyumba zaidi ya 4 zimeharibiwa kabisa maeneo ya kigogo darajani,wakazi wanajaribu kutoa mabaki ya matofali Huyu bwana kaamua kuchukua tahadhari mapema.Anahama tabata dampo

Posted by Bigie
on 5:06 AM.
Filed under
JAMII
.
You can follow any responses to this entry through the
RSS 2.0