BAADA YA FISHCRAB, PRODUCER LAMAR AJA NA FILMATIC


Producer na mshindi wa tuzo za Kili Lamar wa Fishcrab ameamua kuonesha kuwa si uandaaji wa muziki pekee anaouweza bali kamba yake ni ndefu zaidi ya hapo ilipomfikisha.


Mpishi huyo wa midundo ya ukweli nchini, amefungua kampuni mpya chini ya himaya yake ya Fishcrab iitwayo Filmatic.

Akiwa muongozaji mkuu na mchukua picha, mpaka sasa Lamar na timu nzima ya Filmatic ameshatengeneza video tano.

Jana kupitia ukurasa wa Twitter alisema amemaliza kushoot video ya wimbo mpya wa rapper Jaffarai uitwao ‘Tembea Nami’ aliomshirikisha ndugu yake wa Kenya mwanadada Naziz.

“Done filming farrai n naziz neu vid tembea na mi can’t wait the edit n color grade!” alitweet.

Kuhusu Filmatic kujiingiza kwenye utengenezaji wa filamu, Lamar amesema hiyo itategemea kama akipata bajeti ya kutosha.

Posted by Bigie on 3:28 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.