Natafuta Dancers Wa Kike Kwa Muda Mrefu Ila Bado Kupata Wenye Viwango Vya Kimataifa: Diamond Platnumz.
Posted by Bigie burudani 9:25 PMLicha ya kuonekana na madansa wa kike katika jukwaa la Fiesta 2014 Mwanza, Diamond anasema hajabahatika kumpata dansa wa kike mwenye vigezo anavyovitaka.
“Sina madansa wa kike pale wawili ni wa Vanessa naweza sema wote si
wangu, zamani nilikuwa na madansa wa kike, lakini kwa sasa Tanzania tuna
upungufu kwenye muziki wa Bongo Fleva na muziki wa bendi kuna madansa
ambao wamebobea kucheza muziki wa dansi pekee. Nilitamani kuwa na
madansa wa kike zamani lakini ilishindikana maana kuwapata ni ngumu
sana,” anasema na kuongeza:
“Mpaka sasa bado natafuta madansa wa kike sijawapata, nahitaji dansa wa
kike ambaye anajua, awe anajiamini afuatilie madansa wa nje wanachezaje,
awe na unyamwezi kidogo ni ngumu sana, awe mbunifu afuatilie muziki wa
nje na vitu kama hivyo. Kwa hiyo nikatamani nifanyaje nikaamua kuazima
madansa wa watu nifanye nao shoo,” anasema.
Akiwazungumzia madansa wake wa kiume ambao ni sita, Diamond anasema ni
madansa wanaolipwa pesa ndefu ukilinganisha na madansa wote Afrika
Mashariki.
"Siwezi kusema nawalipa kiasi gani itakuwa kama nawavua nguo, lakini
hakuna madansa wanaolipwa vizuri kama wangu Afrika Mashariki, ikiwa bei
inaongezeka na mimi nawaongeza katika malipo yao. Wako sita kwa kweli
nimetoka nao mbali tangu ‘Kamwambie’ mwaka 2009, nimekua nao kifikra,
kiumri na kiakili na kuona kwamba hawa ni mzigo wangu mimi na wanafanya
kazi pamoja na mimi, wale ni mafanikio yangu wana msaada mkubwa sana
pengine nisingekuwa hapa bila wao,” anasema.
Hata hivyo, anaweka wazi kwamba linapofika suala la shoo za nje, huwa
inategemea ni wapi kwani shoo zingine hairuhusiwi kwenda na madansa wote
hivyo huwa anawabadilisha kwa zamu.
Katika mahojiano hayo maalum na Mwananchi, superstar huyo alisema kuwa kwasasa muziki wa Bongofleva unakubalika nje ya nchi tofauti na zamani.
HAYA NDO MASWALI MATATU NILIYO MUULIZA LINAH
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 10:32 AM1.Ni kitu gani unafanya ukiwa peke yako chumbani?
Huwa najiangalia sana kwenye kioo ni "ugonjwa" wangu.
2.How many panties do you have?
Nyingi sana kwani si unajua mimi mwanamke, nataka nitafute kabati lake kabisa.
3.Wakati gani huwa unasema uongo zaidi?
Nikiwa na show nyingi kwa wakati mmoja na zote nataka niwahi.
New Song: Chidi Beenz ft Kahdija Kopa – Nampenda Sana
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 10:18 AMMambo vipi!! Hiyo ni nyimbo yangu nlio release hivi recently nimefanya na Khadija Kopa.
La familia. Chuuma.
New Song: Bandago ft Banana Zorro & Maulo – Achana na Demu Wangu
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 10:17 AMHi peeps!!!!
Tongwe Records brings back the good old days. Old Skool is back and this time with a full swing.
BANDAGO ft BANANA ZORRO come with old banger ACHANA NA DEMU WANGU, produced by J-Ryder of Tongwe Records, a track that disses a new skool dude (Banana) trying to hit Bandago’s chick with a fake old skool swag. What happens next…listen for yourself. As they say music never dies….we’re getting in touch with what really brought us to where we are today… OLD SKOOL HIP HOP
Peace y’all
J-Murder
New Song: Saraha – Jambazi
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 10:14 AMMSANIII NA MBUNGE WA MBEYA MJINI(CHADEMA) JOSEPH MBILINYI(SUGU) NA MBUNGE WA ARUMERU MASHARIKI (CHADEMA) JOSHUA NASARI, VINEGA, JUMA NATURE, PROF JAY WAFUNIKA DAR LIVE
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 11:02 AM Sugu akiwarusha mashabiki waliofurika ndani ya Dar Live usiku wa kuamkia leo.
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari nae akitoa 'verse' kuupamba usiku wa Sugu ndani ya Dar Live.
Sugu na Mkoloni wakizidi kuwadatisha mashabiki.
Profesa Jay akiwapa burudani mashabiki wa Dar Live.
...Akiwasabahi mashabiki wake.
Mapacha kutoka kundi la Vinega wakiiteka steji ya Dar Live.
Suma G nae alikuwepo kuupamba usiku huo.
Juma Nature na kundi lake la Wanaume Halisi likifanya makamuzi stejini.
....Wanaume kazini.

Kundi la Naukala Ndima likifanya vitu vyake stejini.

Bendi ya Chuchu Sound nayo ilifanya makamuzi katika tamasha hilo la Usiku wa Sugu.
Mbunge wa Kinondoni (CCM), Idd Azzan akiwasalimia mashabiki wa Dar Live.
Nyomi iliyohudhuria Usiku wa Sugu.
Baadhi ya mashabiki wakiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Sugu.
-
Msanii mahiri wa HIP HOP ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi 'Mr II' a.k.a Sugu, jana alizikonga nyoyo za mashabiki wake waliofurika ndani ya ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam kwa kufanya makamuzi ya hatari katika tamasha la Usiku wa Sugu. Sugu alisindikizwa na Juma Nature, Profesa Jay, Vinega, Mkoloni na wengineo wengi kwenye shoo hiyo iliyokuwa ya aina yake.
ROMA MKATOLIKI AKIKAMUA KWENYE UZINDUZI WA HUDUMA MPYA YA AIRTEL (SUPA 5) MOROGORO
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 10:57 AMROMA AKIPERFORM LIVE
ACCESS GRANTED: CHECK OUT BEHIND THE SCENE PICS ZA VIDEO MPYA YA AY IN SOUTH AFRICA
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 9:57 AM Few days ago Tzee number one hustler artist Ambwene Yessaya aka AY ali-jet out of the country akiwa na producer wa MJ Records - Marco Chali kuelekea South Africa kwa ajili ya kutengeneza video ya ngoma mpya ya AY ambayo amempa shavu Marco.
The video is reported to cost AY more than $28,000 for production na matumizi mengine.
Wapekuzi tumefanikiwa kupata pics za matukio yaliyokuwa yakifanyika nyuma ya camera wakati wa utengenezwaji wa video hiyo and here we are, granting you the access to check out what went down in SA.
The video is reported to cost AY more than $28,000 for production na matumizi mengine.
Wapekuzi tumefanikiwa kupata pics za matukio yaliyokuwa yakifanyika nyuma ya camera wakati wa utengenezwaji wa video hiyo and here we are, granting you the access to check out what went down in SA.
BARAJA: MSANII ALIYEGEUKA OMBAOMBA BAADA YA KUMZINGUA LAMAR
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 1:28 AMUtapata picha gani pale msanii uliyemuona kwenye video kali iliyotengenezwa na Karabani huku mashairi yake yakielea juu ya mdundo ‘heavy’ wa mpishi Lamar, akisimamisha gari lako na kukuomba umsaidie mia tano akauone wa mchana (akale)? Surprise bila shaka!
Na kama ndio ulikuwa na ndoto za kujaribu bahati kwenye muziki, ndoto hiyo inaweza kuyeyuka kama glucose mdomoni.
Situation hii imemtokea kwa kijana aitwaye Baraja. Lamar aligundua kipaji chake na kujitolea kumsaidia kwa kumfanyia ngoma bure! Baraja kijana kutoka Shinyanga alikuja Dar kama ombaomba na katika pitapita akaligusa sikio la Lamar ambaye alimsaidia kurekodi wimbo uitwao ‘Maumivu.’
Lamar hakuishia hapo, aliamua kuingia mfukoni mwake na kuchomoa laki kadhaa kumlipia video kwa Karabani.
Mwisho wake ni sad story! Baada ya airtime kadhaa kwenye radio na kwenye TV, dogo si akajiona supastaa! Lamar atamwambia nini wakati mtaani wanamwambia wameiona video yake inabang na wanamkubali kinoma!
“Anasema mimi namdhulumu pesa zake, eti naenda kuperfom nyimbo yake kwenye matamasha!” Lamar alitweet kujibu swali la mwandishi wetu kuhusu issue hiyo.
Producer huyo mwenye umri mdogo na ambaye anachukua credits za kumrudisha Mr.Nice kwenye game, aliona isiwe tabu na kusitisha umeneja kwa Baraja.
Mpaka unaisoma story hii ni kwamba Baraja mwenye miaka 15, sasa hivi yupo mitaa ya Dar es Salaam akitembeza bakuli kuomba chochote ili amhudumie bosi tumbo, shughuli iliyomleta Dar.
Poor Baraja!
MTANZANIA AFUNGASHAVIRAGO TUSKER PROJECT FAME 5
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 1:23 AMJana mwakilishi wa Tanzania katika mashindano ya kusaka vipaji vya kuimba ya Tusker Project Fame msimu wa tano Linius ameyaaga mashindano hayo.
Akijaribu kuwashawishi majaji na walimu kwa mara nyingine baada kuwekwa kwenye probation, Linius aliimba wimbo wa Diamond ‘Mbagala’ ambao hata hivyo haukumwokoa.
Linius sio peke yake aliyeyaaga mashindano hayo kwani ameungana na wenzake wawili Brian Luzinda wa Uganda na Diana Teta wa Rwanda.
Washiriki walioponea chupuchupu usiku wa jana ni Doreen Muchiri wa Kenya, Nancy wa Sudan Kusini na Joe wa Burundi.
KWA NINI NI MUHIMU KWA WASANII WA TANZANIA KUJIUNGA NA TWITTER
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 1:21 AMTangu kuanzishwa kwa ulimwengu wa mitandao ya kijamii, mambo mengi yamerahisishwa zaidi. Mitandao hiyo husasan Facebook na Twitter imeongeza mawasiliano baina ya watu wanaofahamiana, kujenga urafiki, uchumba na mawasiliano kati ya makampuni na wateja yamekuwa rahisi zaidi.
Kwa Tanzania hata hivyo, Facebook ndio mtandao maarufu zaidi kuliko Twitter. Pamoja na urahisi huo wa Facebook bado kuna wasanii wengi ambao roho zao ni ngumu kujiunga kutokana na kutojua faida zake. Kwa upande wa Twitter ambayo wengi hushindwa kuielewa vizuri, siku za hivi karibuni imetokea kutumiwa zaidi na makampuni na watu maarufu kuliko Facebook.
Wasanii wengi wachanga na waliofanikiwa wameshindwa kuitumia fursa ya mtandao huu muhimu katika kujitangaza na kuwa karibu na wadau, hali inayowafanya wazikose fursa nyingi.
Post za Twitter hasa zile zilizoandikwa na msanii mwenyewe kwa mkono wake huwakilisha kauli yake mwenyewe inayoenda kwa mashabiki wake. Sio lazima tena kusubiri interview ya radio ili awaambie albam yake ipo sokoni tayar au kutoa habari sake zozote zinazomhusu msanii mwenyewe.
Fareed Kubanda aka Fid Q ameanzisha utaratibu wa kila weekend kuwapa nafasi watu wanaomfollow ili wamuulize maswali na yeye hujibu yote. Kitu hiki kimempa umaarufu kwenye mtandao huo huku wengi wakijua masuala mbalimbali yanayomhusu na si mpaka kusubiri ahojiwe na radio. Mashabiki wana uwezo wa kumuuliza maswali ambayo hayaulizwi na watangazaji kwenye interview.
Kutokana na ukweli huo, Twitter ni mtandao usioepukika kwa wasanii ama bendi wanaotaka kuongeza nafasi za kuwa wanamuziki wenye mafakinio kwenye biashara ya muziki.
Mwenyekiti mtendaji wa mtandao wa Headliner.fm (mtandao mahsusi wa marketing kwa wanamuziki) Mike More anasema Twitter ni ‘njia iliyonyooka kuelekea kwa mashabiki.’
Faida kubwa na ya wazi ya wasanii kutumia Twitter ni uwezo wake wa kutoa mawasiliano ya moja kwa moja na mashabiki. Twitter imewasaidia sana wasanii kama AY na Diamond miongoni mwa wengine waliojiunga, kuongeza idadi yamashabiki nje ya Tanzania.
Wasanii wengine wamepata show nyingi za nje kupitia Twitter. Uzoefu unaonesha pia kuwa wasanii wengi wako active zaidi Twitter kuliko Facebook kutokana na mitandao hiyo kutofautiana mfumo na aina ya watumiaji. Msanii aliyepo Facebook pekee hukosa fursa ya kubadilishana mawazo na wasanii wengine kwakuwa wao hutumia muda mwingi Twitter.
Ni rahisi sana kwa msanii mchanga kujitangaza Twitter hasa pale anapotumia mgongo wa msanii mkubwa. Kwa mfano msanii mchanga anaweza kutweet kitu ambacho kikimpendeza msanii kama AY mwenye followers takriban 15,000, anaweza kukiretweet na kikasomwa na watu wote wanaomfuata ambao watamtambua msanii huyu huku wengine wakiamua kumfollow. Hili huwezi kulipata Facebook.
Ukishajiunga na Twitter msanii unapaswa kuzingatia yafuatayo:
Kuwa mhudhuriaji.
Ukishaingia Twitter, unahitaji kuanza kutweet. Kama mitandao mingine ya kijamii, utaielewa kwa haraka kama ukiwa mtumiaji mzuri.
Ukishafungua profile ya Twitter unatakiwa kuamua kama utakuwa ukitweet kama msanii ama member wa kundi/bendi fulani. Ni wazi kama wewe ni solo artist chaguo hili ni kwajili yako na rahisi zaidi kukuunganisha na mashabiki.
Hata hivyo inapendekezwa kuwa kama utafungua akaunti ya bendi tweet zenu zioneshe ‘ninyi’ mmesema jambo ama kama ni mmoja akiandika basi ataje jina lake pale inapotakiwa.
Hakikisha tu kuwa mtu atakayewajibika kusimimamia akaunti awe anayeweza kujichanganya, mcheshi, funny n.k.
Andika historia yako
Sehemu ya kuandika historia yako umepewa meneno machache sana hivyo yatumie vizuri kuandika maneno yatakayorahisha wewe upatikane kirahisi kwenye search engines (Search Engine Optimisation). Hivyo unatakiwa kuelezea kwa makini unachofanya na muziki wako kwa maneno yatakayowasaidia watu kukupata kirahisi kama wakiserch jina lako kwenye Google.
Anza kufollow
Wafuate marafiki zako kwanza, watu wanaokuvutia, watangazaji, madj, radio na watu wengine wote wanaokuvutia. Epuka kasumba kuwa wewe ni supastaa hivyo hutakiwi kufollow watu.
Utweet kwa kiasi gani?
Mara kwa mara ni vizuri zaidi. Tweet moja kwa siku ni bora kuliko tweets tano kwa siku halafu unakaa mwezi mzima.
Jaribu kufikiria kama vile upo kijiweni mkiongea na washkaji.
Ni ngumu kujua kama unazidisha. Kama unahisi unazungumzia kila tukio unalofanya na watu wanaokufuata hawaoneshi kujibu basi hapo huenda umepitiliza. Mfano “Nimekula ugali na nimeshiba sasa nataka kulala” Unadhani tweet hii itavutia majibu?
Jichanganye kwenye mazungumzo ya wengine
Sio lazima iwe kuhusu wewe tu. Ni kuhusu wao pia na mazungumzo unayofanya nao. Hiyo ndio kazi ya alama ya ‘@’. Pale mtu anapotaka kuchangia kitu ulichotweet atatumia alama hiyo.
Hii ni nzuri kwakuwa watu wataona umejibiwa. Na mtu ambaye hajakufollow anaweza kuvutiwa kufanya hivyo ili akujue zaidi.
Unaposhiriki kwenye mijadala mbalimbali inakufanya uongeze uhusiano na mashabiki na kujipatia wengine zaidi.
Kwa upande mwingine unaporukia jambo ulilovutiwa nalo kwa mtu unayemfollow na kuchangia mada ama mazungumzo yake inakupa credit zaidi.
Hivyo ndivyo watu watu wanataka kuona sio zile tweet za “Angalia website yangu blah blah blah”
Hata hivyo usipitilize ku‘@reply’. Kama umejikuta umeingilia mazungumzo ya watu na ukaona majibu unayopata ni ya aina hii: (‘I agree’ / ‘That’s funny’, Lmao ama LOL) basi jua umezidisha. Hii inakufanya uonekane unajipendekeza, uko shallow na kiwango cha kelele na kurukia mazungumzo ya wengine kwa watu wanaokufuata kitasababisha wakuunfollow.
Sambaza masuala muhimu
Hii ni njia nzuri sana kuitumia kwenye Twitter. Unaweza kuwa unaweka link ya website ama radio ya online inayocheza nyimbo zako na vitu ambavyo vinakuvutia na wale wanaokufollow wanavipenda pia.
Retweet
Kutweet tena kile alichotweet mtu baada ya kukipenda ni kitu cha msingi kwenye mtandao huu.
Hii itawafanya watu wakufollow zaidi na kuamini kuwa unataka kusambaza mambo mazuri na si kupromote muziki wako pekee.
Tweets za watu ambao unaweza kuzire-tweet zinaweza kuwa za wasanii wenzako kupromote show zao, uzinduzi wa albam nk! share the love!
Faida yake ni kuwa wale ambao utakuwa unaretweet mambo yao watalipa fadhila pia kwa kufanya hivyo pale utakapokuwa unapromote kitu chako.
Hata hivyo usiretweet kila linalosemwa. Hii itakufanya uonekane mtu usiyeweza kupembua mambo.
Usisahau lakini kuwa mtu anaporetweet jambo lako tena kwa wafuasi wengi kuliko ulionao wewe, anapaswa kuambiwa ‘Asante.’
Direct Message
DM mara nyingi hutumiwa vibaya na inaweza kukuletea shida.
Inaweza kuwa njia nzuri kwa mazungumzo ya faragha lakini unapaswa kuwa makini nayo.
Mwisho kama msanii bado hujajiunga na Twitter fahamu kuwa unapitwa na mengi na fanya haraka kujiunga kabla hujachelewa.
BAADA YA FISHCRAB, PRODUCER LAMAR AJA NA FILMATIC
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 3:28 AMProducer na mshindi wa tuzo za Kili Lamar wa Fishcrab ameamua kuonesha kuwa si uandaaji wa muziki pekee anaouweza bali kamba yake ni ndefu zaidi ya hapo ilipomfikisha.
Mpishi huyo wa midundo ya ukweli nchini, amefungua kampuni mpya chini ya himaya yake ya Fishcrab iitwayo Filmatic.
Akiwa muongozaji mkuu na mchukua picha, mpaka sasa Lamar na timu nzima ya Filmatic ameshatengeneza video tano.
Jana kupitia ukurasa wa Twitter alisema amemaliza kushoot video ya wimbo mpya wa rapper Jaffarai uitwao ‘Tembea Nami’ aliomshirikisha ndugu yake wa Kenya mwanadada Naziz.
“Done filming farrai n naziz neu vid tembea na mi can’t wait the edit n color grade!” alitweet.
Kuhusu Filmatic kujiingiza kwenye utengenezaji wa filamu, Lamar amesema hiyo itategemea kama akipata bajeti ya kutosha.
Akiwa muongozaji mkuu na mchukua picha, mpaka sasa Lamar na timu nzima ya Filmatic ameshatengeneza video tano.
Jana kupitia ukurasa wa Twitter alisema amemaliza kushoot video ya wimbo mpya wa rapper Jaffarai uitwao ‘Tembea Nami’ aliomshirikisha ndugu yake wa Kenya mwanadada Naziz.
“Done filming farrai n naziz neu vid tembea na mi can’t wait the edit n color grade!” alitweet.
Kuhusu Filmatic kujiingiza kwenye utengenezaji wa filamu, Lamar amesema hiyo itategemea kama akipata bajeti ya kutosha.
LADY JAYDEE NI MTU WA TATU KWA UMAARUFU NCHINI TANZANIA KWENYE MTANDAO
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 8:35 PMKwa mujibu wa mtandao wa starcount.com, leo Judith Wambura aka Lady Jaydee ni mtu wa tatu maarufu zaidi nchini Tanzania kwenye mitandao ya kijamii.
Mtandao huo uliozinduliwa rasmi juzi (May 31) ni mkubwa zaidi wa aina hiyo wenye uwezo wa kusoma tabia za watu bilioni 1.5 duniani kote.
Charts hizo zinajumuisha mambo yote kuanzia makampuni, wanamichezo, wanamuziki, vyombo vya habari n.k na kuviweka pamoja kwenye chart ambayo hubadilika kila siku.
Kwa leo Jaydee amekamata pia nafasi ya 34 kwa umaarufu mtandaoni kwa upande wa Afrika Mashariki na kwa dunia nzima amekamata nafasi ya 19,062.
Katika chart hiyo upande wa Tanzania nafasi ya pili imekamatwa na Hasheem Thabeet, nafasi ya nne ni mtandao wa Jamii Forums, (5) Mwananchi Communications, (6) Rais Jakaya Kikwete, (7) Air Tanzania, (8) ZanAir, (9) Michael Mlingwa, (10) Muhidin Issa Michuzi
MISIMAMO YA ROMA ILIMFANYA AFUKUZWE SHULE
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 8:00 PMIbrahim Musa aka Roma kama watu wanamvyomtambua, hakuanza leo hii kuwa na misimamo mikali dhidi ya utawala.
Msimamo mkali ulimcost masomo pamoja na wenzake kadhaa baada ya kufukuzwa shule alipokuwa katika shule ya Sekondari ya Old Moshi.
Hatua hiyo ilimfanya Roma ambaye jina lake hilo kwa mujibu wake linaundwa na herufi nne za kaka na dada zake Rashid, Omar, Maimuna na Asha, ilimfanya arudi kwenye shule ya Sekondari ya Usagara aliyosoma miaka minne ya mwanzo ili kumalizia masomo yake ya kidato cha sita.
Roma anayejulikana kwa uvaaji wa rozali anasema mwaka 2007 ndipo aliamua kufanya muziki baada ya kuvutiwa na Profesa J.
Rhymes of Magic Attraction, kirefu kingine cha jina lake, kikathibitika kutokana na uandishi wake wenye meneno makali.
Anasema wimbo wake uitwao Pastor, ndio uliompa matatizo zaidi baada ya kuonekana umekaa kidini na kupendelea zaidi dhehebu la Roman Catholic kutokana na mstari unaosema, “Zitakuja dini zote lakini RC itabaki.”
Radio nyingi ziligoma kuucheza wimbo huo na hivyo kudumu kwa miezi minne pekee.
Wimbo Mathematics ndio uliompa umaarufu maradufu baada ya kumpa tuzo mbili za Kili, mwanamuziki bora wa Hip hop wa mwaka 2011 na wimbo bora wa Hip Hop wa mwaka 2011.
Na sasa akiwa anajiandaa kuachia documentary yake, albam yake iliyoshirikisha wasanii kama Jos Mtambo, Izzo B, Mwana FA, Kala Jeremiah, JCB, Chiku Keto na wengine iko mbioni kutoka.
KIM KARDASHIAN ROCKS ESQUIRE LATIN AMERICA
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 4:30 PMPICHA MBILI ZA MSANII MARYA WA KENYA AKIPERFORM KWENYE MSETO CAMPUS TOUR!
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 4:29 PMEXTRA BONGO YAPIGA SHOW YA NGUVU NDANI YA UKUMBI WA ZHONGHUA
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 4:19 PMDIAMOND: "NAMSHUKURU WEMA SEPETU KWA KUNIFUNDISHA KIINGEREZA"
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 10:35 AM
Diamond mapema leo akiwa katika studio za Clouds FM kwa ajili ya interview.
---
Kwenye kipindi cha XXL leo kinacho rushwa na Clouds Fm msanii Diamond aliulizwa ni kwa vipi aliweza kujielezea vizuri sana kwa lugha ya Kingereza baada ya performance yake kwenye Big Brother StarGame maana wengi huwa wanashindwa ifikapo hatua hiyo Diamond alifunguka na kukiri kwamba mrembo Wema Sepetu amechangia kiasi kikubwa kwake kujua lugha hiyo na kusema napenda kumshukuru 'WEMA ENGLISH COURSE'...... kusema ukweli nilifurahi sana kusikia hivyo maana pamoja na mascandal yao yote angalau Diamond ameweza kuongelea upande mzuri wa Wema na ni jinisi gani ameweza kuchangia mafanikio yake kwa kiasi flani.
Wakati huo huo Diamond pia ameongela tour yake ambayo anatarajia kuifanya nchini Marekani baadae mwaka huu na nyumba anyo jenga Tegeta ambayo amekiri mpaka sasa ametumia karibia Tshs milioni 69. Nyumba ni ya kisasa, ina vyumba vya kulala vinne, vitatu vyote master, kuna studio, jiko, choo, bafu nk. Pamoja na nyumba hiyo kuna zingine pia ambazo hakupenda kuongelea ila I hope and I'm sure kuna siku atafunguka.
Tunapenda kumtakia kila la kheri Diamond na Big Up to mrembo Wema Sepetu kwa msaada alio mpatia Diamond kwa kumfundisha Kingereza.
Image credit: Millardayo
Shetta ft Diamond - Nidanganye (Official Video)
VIDEO YA "LALA SALAMA" YA DIAMOND IKO NBIONI KUTOKA
Posted by Bigie burudani, habari za kitaifa 10:21 AMLala Salama, wimbo unaobeba jina la albam ya pili ya Diamond Platnumz umehit mtaani bila hata kuachiwa redioni.
Si jambo la kushangaza kumsikia mtoto mdogo akiuimba wimbo huo mstari wa kwanza hadi wa mwisho bila kukosea.
Ujumbe mahsusi uliomo kwenye wimbo unaowasilishwa kwa sauti tamu, yenye upendo uliozungukwa na uchungu na kusindikizwa na ala nzuri, ni sababu zilizoufanya wimbo huo upendwe na watu wa kila rika.
Lakini kwa wanaume ambao wamewaacha wake ama wachumba zao vijijini/nyumbani na kwenda kutafuta maisha mjini, wana kila sababu za kuupenda wimbo huo kwakuwa unaziwakilisha hisia na mawazo waliyonayo juu yao (familia) na jinsi wanavyohangaika mjini.
Na sasa Diamond ameanza kushoot video ya wimbo huo ambao ni muendelezo wa wimbo wake uitwao Nitarejea aliomshirikisha mwanadada Hawa.
Nitarejea ni wimbo uliyoyagusa maisha ya wengi akiwemo Mheshimiwa Zitto Kabwe ambaye juzi alimuuliza swali, “nini kilikuwa kwenye mawazo yako ktk wimbo wa #NITAREJEA ? Whats the story behind? Whats the thinking behind?
Diamond alijibu, “Dah! Ni Mungu tu mkuu,ila niligundua wanaume wengi wa mikoani huja Dar na wa Dar huenda nje za nchi kutafuta Maisha na kuacha familia.”
Mheshimiwa Kabwe akachombeza, “Halafu hawarudi. Nataka kuona ubunifu wako after that. ‘Nimerejea’ au ‘sikutaki tena!
Ndipo Diamond kupitia swali hilo akawapa habari njema wapenzi wa ‘Lala Salama’ kuwa video ipo mbioni kuja kwa kumjibu Mhe.Kabwe, “LOL! Ipo tayari inaitwa “LALA SALAMA” ni muendelezo wa Nitarejea ambayo nashut Video sasa, Ntakutumia BBM uiskie”
Bahati nzuri Zitto Kabwe ameshaisikia LALA SALAMA na tunaamini kausikia ubunifu wa mshindi huyo wa Tuzo za Kili.
Kwa ratiba ngumu aliyonayo msanii huyu mwenye mafanikio makubwa katika kipindi kifupi cha career yake inayohusisha show, kurekodi, kushoot video, mahojiano na vyombo vya habari na maisha binafsi, hatushangai akiandika, “Been soo busy dah, I think I need a vacation!
You are right young man! You really need a vacation!
.
Featured Post
NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne ambayo ni Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...







