WEMA AFANYA KUFURU MPYA


WEMA Isaac Sepetu ‘Pedeshee Mwanamke’, amefanya kufuru mpya baada ya kuvuta mkoko wa maana wenye thamani ya Sh. milioni 38 na kumpa mama yake, Miriam Sepetu ule usafiri aliokuwa akitumia wa Toyota Lexus Harrier.

Wema ambaye ni tishio katika filamu za Kibongo na umodo alifanya tukio hilo Mei 25, mwaka huu kwa kile alichodai kuwa aliona mama yake anateseka na usafiri kwani siku chache gari la mzazi wake huyo alilokuwa akitumia lilipata hitilafu.


AINA YA GARI
“Ni Toyota Mark X. Muda mrefu nilipanga kununua gari la kifahari lakini kitendo cha kuharibika kwa gari la mama kimechochea mimi kununua gari hili,” alisema Wema.


ANAPATA WAPI JEURI?
Ni kitambo sasa, Wema kama ilivyo kwa Jacqueline Wolper, amekuwa hana shida ndogondogo kwa kuwa mkwanja anao wa kutosha na kwa mujibu wa rafiki yake wa karibu, amenunua gari hilo ili kuwathibitishia kuwa fedha siyo tatizo kwake kwani ana ‘mnene’ anayemuwezesha.

Posted by Bigie on 10:35 AM. Filed under . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.