"SADAKA ILINIFANYA NIKIMBIE KANISA".....JINI KABULA


Mwigizaji wa filamu Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’  hivi  karibuni alidai kuwa siku za nyuma baada ya kuzongwa na matatizo aliamua kumrudia Mungu wake kwa kuokoka katika kanisa moja maeneo ya Mwenge akiamini kuwa anaenda kupata faraja lakini alichokutana nacho huko ikibidi kurudi katika kanisa lake la awali.

“Unajua kuna wakati mtu unapokabiliwa na mitihani unaangalia njia sahihi ya kutafuta utatuzi, kwa wakati huo njia sahihi kwangu niliamua kuokoka na kujiunga na kanisa moja Mwenge, sasa kilichonikimbiza ni pale Mchungaji aliposema Mungu atakubariki ukitoa fedha nyingi kama sadaka,” alisema Kabula.

Jini Kabula kutokana na mahubiri hayo ya kuhimiza sadaka kubwa kuwa ndio kigezo cha kupata Baraka aliona kumbe maskini wanaosali katika kanisa lile wanapoteza muda kwani hawezi kuokolewa kwa sababu ya sadaka zao kuwa ndongo, Kabula akaona ni bora kurudi katika dhehebu lake la Sabato.

Posted by Bigie on 3:39 PM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.