BANANA AKERWA NA MIMBA YA DADA YAKE






MMILIKI wa B-Band, Banana Zorro amefunguka la moyoni kuwa, mimba aliyopata dada’ke, Maunda Zorro mwaka jana ilikuwa ikimkera hivyo akamnunia.
Akisemezana na kituo kimoja cha televisheni cha jijini Dar juzikati, Banana alisema kuwa kwa kipindi kile hakutarajia kama mdogo wake angepata ujauzito ndiyo maana baada ya kupata taarifa hiyo alikasirika.

“Kusema ukweli hata yeye baada ya kupata ujauzito hakuweza kuniambia moja kwa moja, akamwambia mke wangu, nilikereka sana lakini nilimsamehe baada ya kupata mtoto,” alisema Banana.

Posted by Bigie on 4:06 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.