"NAMPENDA BWANA MISOSI KWA SABABU HANA DHARAU NA ANAJIHESHIMU".....AMANDA

MSANII wa Filamu za Kibongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’ amefunguka  kuwa heshima aliyonayo staa wa Muziki wa Bongo fleva, Joseph Lushalu `Bwana Misosi’ ndiyo iliyomfanya ampe penzi lake.

Akiongea na mwandishi wa habar hii, Amanda alisema yeye siyo kama wanawake wengine ambao wanavutiwa na sauti,swaga na  sura, bali amempenda Bwana Misosi kutokana na heshima aliyonayo katika jamii.
 

“Bwana Misosi hana dharau, anawaheshimu wakubwa na wadogo pia ana mapenzi ya dhati tofauti na wanaume wengine wa siku hizi,” alisema.

Aidha, alisema kuwa kutokana na hivyo anampenda mpenzi wake huyo kuliko kitu chochote na anamuomba Mungu ayaendeleze  mapenzi yao ya dhati ili wadumu milele.

Posted by Bigie on 1:10 AM. Filed under , , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.