LUCY KOMBA APATA SHAVU LA KUFANYA FILAMU NCHINI DENMARK


 
STAA wa sinema za Bongo, Lucy Francis Komba amekula shavu la kufanya filamu nchini Denmark kwa miezi mitatu hadi mwakani.


Akichonga na safu hii juzikati, jijini Dar akiwa njiani kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar ambako aliondoka na Ndege ya Scandinavia Airways, Lucy alisema:


“Ni kweli nasafiri, nakwenda Denmark kucheza filamu. Nitakuwa kule kuanzia Oktoba hii, Novemba, Desemba na Januari.”


Miezi ya hivi karibuni, Lucy amekuwa akienda kufanya ‘shooting’ ya filamu nje ya nchi. Katikati ya mwaka huu, alikwenda Ghana, Nigeria na baadaye Burundi.

Posted by Bigie on 12:33 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0
.

Featured Post

NEC ya ahirisha uandikishaji kwa BVR mikoa 4 nchini

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeahirisha zoezi la uandikishaji kwa BVR katika mikoa minne  ambayo ni  Arusha, Kilimanjaro, Manyara pamoja ...

2010 BlogNews Magazine. All Rights Reserved. - Provided by Free Blogger template.